< Proverbios 8 >

1 ¿No clama la sabiduría, y da su voz la inteligencia?
Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
2 En los altos cabezos, junto al camino, a las encrucijadas de las veredas se para;
Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
3 en el lugar de las puertas, a la entrada de la ciudad, a la entrada de las puertas da voces:
Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
4 Oh hombres, a vosotros clamo; y mi voz es a los hijos de los hombres.
Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
5 Entended, simples, la astucia; y vosotros, locos, tomad entendimiento.
Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Oíd, porque hablaré cosas excelentes; y abriré mis labios para cosas rectas.
Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Porque mi paladar hablará verdad, y mis labios abominan la impiedad.
Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 En justicia son todas las razones de mi boca; no hay en ellas cosa perversa ni torcida.
Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Todas ellas son rectas al que entiende; rectas a los que han hallado sabiduría.
Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Recibid mi castigo, y no plata; y ciencia más que el oro escogido.
Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Porque mejor es la sabiduría que las piedras preciosas; y todas las cosas que se pueden desear, no son de comparar con ella.
Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 Yo, la sabiduría, moré con la prudencia; y yo invento la ciencia de los consejos.
Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 El temor del SEÑOR es aborrecer el mal; la soberbia, la arrogancia, el mal camino, y la boca perversa, aborrezco.
Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 Conmigo está el consejo y el ser; yo soy la inteligencia; mía es la fortaleza.
Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Por mí reinan los reyes, y los príncipes determinan justicia.
Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Por mí dominan los príncipes, y todos los gobernadores juzgan la tierra.
Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Yo amo a los que me aman; y los que me buscan me hallan.
Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Las riquezas y la honra están conmigo; sólidas riquezas, y justicia.
Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 Mejor es mi fruto que el oro, y que la piedra preciosa; y mi rédito mejor que la plata escogida.
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 Por vereda de justicia guiaré, por en medio de veredas de juicio;
Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 para hacer heredar a mis amigos el ser, y que yo llene sus tesoros.
katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 El SEÑOR me poseyó en el principio de su camino, desde entonces, antes de sus obras.
Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23 Eternalmente tuve el principado, desde el principio, antes de la tierra.
Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24 Antes de los abismos fui engendrada; antes que fuesen las fuentes de las muchas aguas.
Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25 Antes que los montes fuesen fundados, antes de los collados, era yo engendrada;
Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26 no había aún hecho la tierra, ni las campiñas, ni el principio del polvo del mundo.
Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27 Cuando componía los cielos, allí estaba yo; cuando señalaba por compás la sobrefaz del abismo;
Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
28 cuando afirmaba los cielos arriba, cuando afirmaba las fuentes del abismo;
Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
29 cuando ponía al mar su estatuto, y a las aguas, que no pasasen su mandamiento; cuando señalaba los fundamentos de la tierra;
Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
30 con él estaba yo ordenándolo todo; y fui su delicia todos los días, teniendo solaz delante de él en todo tiempo.
Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
31 Tengo solaz en la redondez de su tierra; y mis solaces son con los hijos de los hombres.
Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32 Ahora, pues, hijos, oídme; y bienaventurados los que guardaren mis caminos.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33 Escuchad al castigo, y sed sabios; y no lo menospreciéis.
Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34 Bienaventurado el hombre que me oye, trasnochando a mis puertas cada día, guardando los umbrales de mis entradas.
Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35 Porque el que me hallare, hallará la vida; y alcanzará la voluntad del SEÑOR.
Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
36 Mas el que peca contra mí, defrauda su alma; todos los que me aborrecen, aman la muerte.
Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.

< Proverbios 8 >