< Proverbios 10 >

1 (Las parábolas de Salomón.) El hijo sabio alegra al padre; y el hijo loco es tristeza a su madre.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Los tesoros de maldad no serán de provecho; mas la justicia libra de la muerte.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 El SEÑOR no dejará hambrear el alma del justo; mas la iniquidad lanzará a los impíos.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 La mano negligente hace pobre; mas la mano de los diligentes enriquece.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 El que recoge en el verano es hijo entendido; el que duerme en el tiempo de la siega es hijo que avergüenza.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 Bendita es la cabeza del justo; mas la boca de los impíos cubre la iniquidad.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 La memoria del justo será bendita; mas el nombre de los impíos hederá.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 El sabio de corazón recibirá los mandamientos; mas el que habla locuras caerá.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 El que camina en integridad, anda confiado; mas el que pervierte sus caminos, será quebrantado.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 El que guiña el ojo acarrea tristeza; y el que habla locuras caerá.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 Vena de vida es la boca del justo; mas la boca de los impíos cubre la iniquidad.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 El odio despierta las rencillas; mas la caridad cubre todas las maldades.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 En los labios del prudente se halla sabiduría; y es vara a las espaldas del falto de entendimiento.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Los sabios guardan la sabiduría; mas la boca del loco es calamidad cercana.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 Las riquezas del rico son su ciudad fuerte; y el desmayo de los pobres es su pobreza.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 La obra del justo es para vida; mas el fruto del impío es para pecado.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 Camino a la vida es guardar el castigo; mas el que deja la reprensión, yerra.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 El que encubre el odio es de labios mentirosos; y el que echa mala fama es loco.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 En las muchas palabras no falta rebelión; mas el que refrena sus labios es prudente.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 Plata escogida es la lengua del justo; mas el entendimiento ( o corazón ) de los impíos es como nada.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 Los labios del justo apacientan a muchos; mas los locos con falta de entendimiento mueren.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 La bendición del SEÑOR es la que enriquece, y no añade tristeza con ella.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 Hacer abominación es como risa al loco; mas la sabiduría recrea al varón de entendimiento.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 Lo que el impío teme, eso le vendrá; mas Dios da a los justos lo que desean.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Cuando pasare el torbellino, el malo no será; mas el justo, fundado para siempre.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 Como el vinagre a los dientes, y como el humo a los ojos, así es el perezoso a los que lo envían.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 El temor del SEÑOR aumentará los días; mas los años de los impíos serán acortados.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 La esperanza de los justos es alegría; mas la esperanza de los impíos perecerá.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 El camino del SEÑOR es fortaleza al perfecto; pero es espanto a los que obran maldad.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 El justo eternalmente no será removido; mas los impíos no habitarán la tierra.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 La boca del justo producirá sabiduría; mas la lengua perversa será cortada.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 Los labios del justo conocerán la voluntad de Dios; mas la boca de los impíos habla perversidades.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

< Proverbios 10 >