< 1 Crónicas 6 >

1 Los hijos de Leví: Gersón, Coat, y Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 Los hijos de Coat: Amram, Izhar, Hebrón y Uziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 Los hijos de Amram: Aarón, Moisés, y María. Los hijos de Aarón: Nadab, Abiú, Eleazar, e Itamar.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 Eleazar engendró a Finees, y Finees engendró a Abisúa;
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 y Abisúa engendró a Buqui, y Buqui engendró a Uzi;
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 y Uzi engendró a Zeraías, y Zeraías engendró a Meraiot;
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 y Meraiot engendró a Amarías, y Amarías engendró a Ahitob;
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 y Ahitob engendró a Sadoc, y Sadoc engendró a Ahimaas;
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 y Ahimaas engendró a Azarías, y Azarías engendró a Johanán;
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 y Johanán engendró a Azarías, el que tuvo el sacerdocio en la Casa que Salomón edificó en Jerusalén;
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 y Azarías engendró a Amarías, y Amarías engendró a Ahitob;
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 y Ahitob engendró a Sadoc, y Sadoc engendró a Salum;
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 y Salum engendró a Hilcías, e Hilcías engendró a Azarías;
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 y Azarías engendró a Seraías, y Seraías, engendró a Josadac.
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 Y Josadac fue cautivo cuando el SEÑOR trasportó a Judá y a Jerusalén, por mano de Nabucodonosor.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 Los hijos de Leví: Gersón, Coat, y Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 Y estos son los nombres de los hijos de Gersón: Libni, y Simei.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 Los hijos de Coat: Amram, Izhar, Hebrón, y Uziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 Los hijos de Merari: Mahli, y Musi. Estas son las familias de Leví, según sus descendencias.
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 Gersón: Libni su hijo, Jahat su hijo, Zima su hijo.
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 Joab su hijo, Iddo su hijo, Zera su hijo, Jeatrai su hijo.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 Los hijos de Coat: Aminadab su hijo, Coré su hijo, Asir su hijo,
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 Elcana su hijo, Ebiasaf su hijo, Asir su hijo,
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 Tahat su hijo, Uriel su hijo, Uzías su hijo, y Saúl su hijo.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 Los hijos de Elcana: Amasai, Ahimot, y Elcana.
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 Los hijos de Elcana: Zofai su hijo, Nahat su hijo,
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 Eliab su hijo, Jeroham su hijo, Elcana su hijo.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 Los hijos de Samuel: el primogénito Vasni, y Abías.
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 Los hijos de Merari: Mahli, Libni su hijo, Simei su hijo, Uza su hijo,
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 Simea su hijo, Haguía su hijo, Asaías su hijo.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 Estos son a los que David dio cargo de las cosas de la música de la Casa del SEÑOR, después que el arca tuvo reposo.
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 Los cuales servían delante de la tienda del tabernáculo del testimonio en cantares, hasta que Salomón edificó la Casa del SEÑOR en Jerusalén; después estuvieron en su ministerio según su costumbre.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 Estos, pues, con sus hijos asistían: de los hijos de Coat, Hemán cantor, hijo de Joel, hijo de Samuel;
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 hijo de Elcana, hijo de Jeroham, hijo de Eliel, hijo de Toa;
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 hijo de Zuf, hijo de Elcana, hijo Mahat, hijo de Amasai;
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 hijo de Elcana, hijo de Joel, hijo de Azarías, hijo de Sofonías;
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 hijo de Tahat, hijo de Asir, hijo de Ebiasaf, hijo de Coré;
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 hijo de Izhar, hijo de Coat, hijo de Leví, hijo de Israel.
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 Y su hermano Asaf, el cual estaba a su mano derecha: Asaf, hijo de Baasías, hijo de Simea;
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 hijo de Micael, hijo de Baasías, hijo de Malquías;
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 hijo de Etni, hijo de Zera, hijo de Adaía;
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 hijo de Etán, hijo de Zima, hijo de Simei;
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 hijo de Jahat, hijo de Gersón, hijo de Leví.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 Mas los hijos de Merari sus hermanos estaban a la mano siniestra, es a saber, Etán hijo de Quisi, hijo de Abdi, hijo de Maluc;
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
45 hijo de Hasabías, hijo de Amasías, hijo de Hilcías;
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 hijo de Amsi, hijo de Bani, hijo de Semer;
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 hijo de Mahli, hijo de Musi, hijo de Merari, hijo de Leví.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 Y sus hermanos los levitas fueron entregados a todo el ministerio del tabernáculo de la Casa de Dios.
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 Mas Aarón y sus hijos ofrecían incienso sobre el altar del holocausto, y sobre el altar del incienso, en toda la obra del lugar santísimo, y para hacer las expiaciones sobre Israel, conforme a todo lo que Moisés siervo de Dios había mandado.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 Y los hijos de Aarón son estos: Eleazar su hijo, Finees su hijo, Abisúa su hijo;
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 Buqui su hijo, Uzi su hijo, Zeraías su hijo;
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 Meraiot su hijo, Amarías su hijo, Ahitob su hijo;
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 Sadoc su hijo, Ahimaas su hijo.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 Y estas son sus habitaciones, por sus palacios y en sus términos, de los hijos de Aarón por las familias de los coatitas, porque de ellos fue la suerte ( en herencia ),
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 que les dieron a Hebrón en tierra de Judá, y sus ejidos alrededor de ella.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 Mas la tierra alrededor de la ciudad y sus aldeas se dieron a Caleb, hijo de Jefone.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Y a los hijos de Aarón dieron las ciudades de Judá de acogimiento, es a saber, a Hebrón, y a Libna con sus ejidos;
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
58 a Jatir, y Estemoa con sus ejidos, y a Hilén con sus ejidos, y a Debir con sus ejidos;
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 a Asán con sus ejidos, y a Bet-semes con sus ejidos.
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 Y de la tribu de Benjamín, a Geba, con sus ejidos, y a Alemet con sus ejidos, y a Anatot con sus ejidos. Todas sus ciudades fueron trece ciudades, repartidas por sus linajes.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 A los hijos de Coat, que quedaron de su parentela, dieron diez ciudades de la media tribu de Manasés por suerte.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 Y a los hijos de Gersón, por sus linajes, dieron de la tribu de Isacar, de la tribu de Aser, y de la tribu de Neftalí, y de la tribu de Manasés en Basán, trece ciudades.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Y a los hijos de Merari, por sus linajes, de la tribu de Rubén, y de la tribu de Gad, y de la tribu de Zabulón, se dieron por suerte doce ciudades.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 Y dieron los hijos de Israel a los levitas ciudades con sus ejidos.
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 Y dieron por suerte de la tribu de los hijos de Judá, y de la tribu de los hijos de Simeón, y de la tribu de los hijos de Benjamín, las ciudades que nombraron por sus nombres.
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 Y a los linajes de los hijos de Coat dieron ciudades con sus términos de la tribu de Efraín.
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 Y les dieron las ciudades de acogimiento, a Siquem con sus ejidos en el monte de Efraín, y a Gezer con sus ejidos,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
68 y a Jocmeam con sus ejidos, y a Bet-horón con sus ejidos,
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 y a Ajalón con sus ejidos, y a Gat-rimón con sus ejidos.
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 De la media tribu de Manasés, a Aner con sus ejidos, y a Bileam con sus ejidos, para los del linaje de los hijos de Coat que habían quedado.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 Y a los hijos de Gersón dieron de la familia de la media tribu de Manasés, a Golán en Basán con sus ejidos y a Astarot con sus ejidos;
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 y de la tribu de Isacar, a Cedes con sus ejidos, a Daberat con sus ejidos,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 y a Ramot con sus ejidos, y a Anem con sus ejidos;
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 y de la tribu de Aser a Masal con sus ejidos, y a Abdón con sus ejidos,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 y a Hucoc con sus ejidos, y a Rehob con sus ejidos.
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 Y de la tribu de Neftalí, a Cedes en Galilea con sus ejidos, y a Hamón con sus ejidos, a Quiriat-jearim con sus ejidos.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 Y a los hijos de Merari que habían quedado, dieron de la tribu de Zabulón a Rimón con sus ejidos, y a Tabor con sus ejidos;
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 y del otro lado del Jordán frente a Jericó, al oriente del Jordán, dieron, de la tribu de Rubén, a Beser en el desierto con sus ejidos; y a Jasa con sus ejidos.
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 Y a Cademot con sus ejidos, y a Mefaat con sus ejidos;
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 y de la tribu de Gad, a Ramot en Galaad con sus ejidos, y a Mahanaim con sus ejidos,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 y a Hesbón con sus ejidos, y a Jazer con sus ejidos.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.

< 1 Crónicas 6 >