< Salmos 88 >

1 Canción: Salmo para los hijos de Coré: al Músico principal: para cantar sobre Mahalath: Masquil de Hemán Ezrahita. OH Jehová, Dios de mi salud, día y noche clamo delante de ti.
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 Entre mi oración en tu presencia: inclina tu oído á mi clamor.
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 Porque mi alma está harta de males, y mi vida cercana al sepulcro. (Sheol h7585)
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
4 Soy contado con los que descienden al hoyo, soy como hombre sin fuerza:
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 Libre entre los muertos, como los matados que yacen en el sepulcro, que no te acuerdas más de ellos, y que son cortados de tu mano.
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 Hasme puesto en el hoyo profundo, en tinieblas, en honduras.
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 Sobre mí se ha acostado tu ira, y me has afligido con todas tus ondas. (Selah)
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 Has alejado de mí mis conocidos: hasme puesto por abominación á ellos: encerrado estoy, y no puedo salir.
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 Mis ojos enfermaron á causa de mi aflicción: hete llamado, oh Jehová, cada día; he extendido á ti mis manos.
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 ¿Harás tú milagro á los muertos? ¿levantaránse los muertos para alabarte? (Selah)
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 ¿Será contada en el sepulcro tu misericordia, ó tu verdad en la perdición?
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 ¿Será conocida en las tinieblas tu maravilla, ni tu justicia en la tierra del olvido?
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 Mas yo á ti he clamado, oh Jehová; y de mañana mi oración te previno.
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 ¿Por qué, oh Jehová, desechas mi alma? ¿por qué escondes de mí tu rostro?
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 Yo soy afligido y menesteroso: desde la mocedad he llevado tus terrores, he estado medroso.
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 Sobre mí han pasado tus iras; tus espantos me han cortado.
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 Hanme rodeado como aguas de continuo; hanme cercado á una.
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 Has alejado de mí el amigo y el compañero; y mis conocidos [se esconden] en la tiniebla.
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.

< Salmos 88 >