< Salmos 76 >

1 Al Músico principal: sobre Neginoth: Salmo de Asaph: Canción. DIOS es conocido en Judá: en Israel es grande su nombre.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
2 Y en Salem está su tabernáculo, y su habitación en Sión.
Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
3 Allí quebró las saetas del arco, el escudo, y la espada, y [tren] de guerra. (Selah)
Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
4 Ilustre eres tú; fuerte, más que los montes de caza.
Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
5 Los fuertes de corazón fueron despojados, durmieron su sueño; y nada hallaron en sus manos todos los varones fuertes.
Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
6 A tu reprensión, oh Dios de Jacob, el carro y el caballo fueron entorpecidos.
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
7 Tú, terrible eres tú: ¿y quién parará delante de ti, en comenzando tu ira?
Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
8 Desde los cielos hiciste oir juicio; la tierra tuvo temor y quedó suspensa,
Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
9 Cuando te levantaste, oh Dios, al juicio, para salvar á todos los mansos de la tierra. (Selah)
wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
10 Ciertamente la ira del hombre te acarreará alabanza: tú reprimirás el resto de las iras.
Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
11 Prometed, y pagad á Jehová vuestro Dios: todos los que están alrededor de él, traigan presentes al Terrible.
Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
12 Cortará él el espíritu de los príncipes: terrible es á los reyes de la tierra.
Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.

< Salmos 76 >