< Salmos 73 >
1 Salmo de Asaph. CIERTAMENTE bueno es Dios á Israel, á los limpios de corazón.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 Mas yo, casi se deslizaron mis pies; por poco resbalaron mis pasos.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 Porque tuve envidia de los insensatos, viendo la prosperidad de los impíos.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Porque no hay ataduras para su muerte; antes su fortaleza está entera.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 No están ellos en el trabajo humano; ni son azotados con [los otros] hombres.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Por tanto soberbia los corona: cúbrense de vestido de violencia.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Sus ojos están salidos de gruesos: logran con creces los antojos del corazón.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Soltáronse, y hablan con maldad de [hacer] violencia; hablan con altanería.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 Ponen en el cielo su boca, y su lengua pasea la tierra.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Por eso su pueblo vuelve aquí, y aguas de lleno les son exprimidas.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 Y dicen: ¿Cómo sabe Dios? ¿y hay conocimiento en lo alto?
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 He aquí estos impíos, sin ser turbados del mundo, alcanzaron riquezas.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Verdaderamente en vano he limpiado mi corazón, y lavado mis manos en inocencia;
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 Pues he sido azotado todo el día, [y empezaba] mi castigo por las mañanas.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 Si dijera yo, Discurriré de esa suerte; he aquí habría negado la nación de tus hijos:
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 Pensaré pues para saber esto: es á mis ojos [duro] trabajo,
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 Hasta que venido al santuario de Dios, entenderé la postrimería de ellos.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Ciertamente los has puesto en deslizaderos; en asolamientos los harás caer.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 ¡Cómo han sido asolados! ¡cuán en un punto! Acabáronse, fenecieron con turbaciones.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 Como sueño del que despierta, así, Señor, cuando despertares, menospreciarás sus apariencias.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 Desazonóse á la verdad mi corazón, y en mis riñones sentía punzadas.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 Mas yo era ignorante, y no entendía: era como una bestia acerca de ti.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Con todo, yo siempre estuve contigo: trabaste de mi mano derecha.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 Hasme guiado según tu consejo, y después me recibirás en gloria.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 ¿A quién tengo yo en los cielos? Y fuera de ti nada deseo en la tierra.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 Mi carne y mi corazón desfallecen: [mas] la roca de mi corazón y mi porción es Dios para siempre.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 Porque he aquí, los que se alejan de ti perecerán: tú cortarás á todo aquel que fornicando, de ti [se aparta].
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Y en cuanto á mí, el acercarme á Dios es el bien: he puesto en el Señor Jehová mi esperanza, para contar todas tus obras.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.