< Salmos 71 >
1 EN ti, oh Jehová, he esperado; no sea yo confuso para siempre.
Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
2 Hazme escapar, y líbrame en tu justicia: inclina tu oído y sálvame.
Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
3 Séme por peña de estancia, adonde recurra yo continuamente: mandado has que yo sea salvo; porque tú eres mi roca, y mi fortaleza.
Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 Dios mío, líbrame de la mano del impío, de la mano del perverso y violento.
Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
5 Porque tú, oh Señor Jehová, eres mi esperanza: seguridad mía desde mi juventud.
Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
6 Por ti he sido sustentado desde el vientre: de las entrañas de mi madre tú fuiste el que me sacaste: de ti será siempre mi alabanza.
Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
7 Como prodigio he sido á muchos; y tú mi refugio fuerte.
Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
8 Sea llena mi boca de tu alabanza, de tu gloria todo el día.
Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
9 No me deseches en el tiempo de la vejez; cuando mi fuerza se acabare, no me desampares.
Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
10 Porque mis enemigos han tratado de mí; y los que acechan mi alma, consultaron juntamente,
Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
11 Diciendo: Dios lo ha dejado: perseguid y tomadle, porque no hay quien le libre.
Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
12 Oh Dios, no te alejes de mí: Dios mío, acude presto á mi socorro.
Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
13 Sean avergonzados, fallezcan los adversarios de mi alma; sean cubiertos de vergüenza y de confusión los que mi mal buscan.
Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
14 Mas yo siempre esperaré, y añadiré sobre toda tu alabanza.
Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
15 Mi boca publicará tu justicia y tu salud todo el día, aunque no sé el número [de ellas].
Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
16 Vendré á las valentías del Señor Jehová: haré memoria de sola tu justicia.
Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
17 Oh Dios, enseñásteme desde mi mocedad; y hasta ahora he manifestado tus maravillas.
Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 Y aun hasta la vejez y las canas; oh Dios, no me desampares, hasta que denuncie tu brazo á la posteridad, tus valentías á todos los que han de venir.
Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
19 Y tu justicia, oh Dios, hasta lo excelso; porque has hecho grandes cosas: oh Dios, ¿quién como tú?
Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 Tú, que me has hecho ver muchas angustias y males, volverás á darme vida, y de nuevo me levantarás de los abismos de la tierra.
Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
21 Aumentarás mi grandeza, y volverás á consolarme.
Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
22 Asimismo yo te alabaré con instrumento de salterio, oh Dios mío: tu verdad cantaré yo á ti en el arpa, oh Santo de Israel.
Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
23 Mis labios cantarán cuando á ti salmeare, y mi alma, á la cual redimiste.
Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
24 Mi lengua hablará también de tu justicia todo el día: por cuanto fueron avergonzados, porque fueron confusos los que mi mal procuraban.
Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.