< Salmos 56 >

1 Al Músico principal: sobre La paloma silenciosa en paraje muy distante. Michtam de David, cuando los Filisteos le prendieron en Gath. TEN misericordia de mí, oh Dios, porque me devoraría el hombre: me oprime combatiéndome cada día.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 Apúranme mis enemigos cada día; porque muchos son los que pelean contra mí, oh Altísimo.
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 En el día que temo, yo en ti confío.
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 En Dios alabaré su palabra: en Dios he confiado, no temeré lo que la carne me hiciere.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 Todos los días me contristan mis negocios; contra mí son todos sus pensamientos para mal.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 Reúnense, escóndense, miran ellos atentamente mis pasos, esperando mi vida.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 ¿Escaparán ellos por la iniquidad? Oh Dios, derriba en tu furor los pueblos.
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 Mis huídas has tú contado: pon mis lágrimas en tu redoma: ¿no están ellas en tu libro?
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 Serán luego vueltos atrás mis enemigos el día que yo clamare: en esto conozco que Dios es por mí.
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 En Dios alabaré [su] palabra; en Jehová alabaré [su] palabra.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 En Dios he confiado: no temeré lo que me hará el hombre.
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 Sobre mí, oh Dios, están tus votos: te tributaré alabanzas.
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 Porque has librado mi vida de la muerte, y mis pies de caída, para que ande delante de Dios en la luz de los que viven.
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.

< Salmos 56 >