< Salmos 23 >

1 Salmo de David. JEHOVÁ es mi pastor; nada me faltará.
Zaburi ya Daudi. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.
2 En lugares de delicados pastos me hará yacer: junto á aguas de reposo me pastoreará.
Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,
3 Confortará mi alma; guiaráme por sendas de justicia por amor de su nombre.
hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Aunque ande en valle de sombra de muerte, no temeré mal alguno; porque tú estarás conmigo: tu vara y tu cayado me infundirán aliento.
Hata kama nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.
5 Aderezarás mesa delante de mí, en presencia de mis angustiadores: ungiste mi cabeza con aceite: mi copa está rebosando.
Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.
6 Ciertamente el bien y la misericordia me seguirán todos los días de mi vida: y en la casa de Jehová moraré por largos días.
Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

< Salmos 23 >