< Salmos 120 >
1 Cántico gradual. A JEHOVÁ llamé estando en angustia, y él me respondió.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Libra mi alma, oh Jehová, de labio mentiroso, de la lengua fraudulenta.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 ¿Qué te dará, ó qué te aprovechará, oh lengua engañosa?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Agudas saetas de valiente, con brasas de enebro.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 ¡Ay de mí, que peregrino en Mesech, [y] habito entre las tiendas de Kedar!
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 Mucho se detiene mi alma con los que aborrecen la paz.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Yo soy pacífico: mas ellos, así que hablo, [me] hacen guerra.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.