< Salmos 109 >
1 Al Músico principal: Salmo de David. OH Dios de mi alabanza, no calles;
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
2 Porque boca de impío y boca de engañador se han abierto sobre mí: han hablado de mí con lengua mentirosa,
kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
3 Y con palabras de odio me rodearon; y pelearon contra mí sin causa.
Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
4 En pago de mi amor me han sido adversarios: mas yo oraba.
Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
5 Y pusieron contra mí mal por bien, y odio por amor.
Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
6 Pon sobre él al impío: y Satán esté á su diestra.
Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
7 Cuando fuere juzgado, salga impío; y su oración sea para pecado.
Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
8 Sean sus días pocos: tome otro su oficio.
Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
9 Sean sus hijos huérfanos, y su mujer viuda.
Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
10 Y anden sus hijos vagabundos, y mendiguen; y procuren [su pan lejos] de sus desolados hogares.
Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
11 Enrede el acreedor todo lo que tiene, y extraños saqueen su trabajo.
Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
12 No tenga quien le haga misericordia; ni haya quien tenga compasión de sus huérfanos.
Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
13 Su posteridad sea talada; en segunda generación sea raído su nombre.
Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
14 Venga en memoria cerca de Jehová la maldad de sus padres, y el pecado de su madre no sea borrado.
Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
15 Estén siempre delante de Jehová, y él corte de la tierra su memoria.
Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
16 Por cuanto no se acordó de hacer misericordia, y persiguió al hombre afligido y menesteroso y quebrantado de corazón, para matar[lo].
Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
17 Y amó la maldición, y vínole; y no quiso la bendición, y ella se alejó de él.
Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
18 Y vistióse de maldición como de su vestido, y entró como agua en sus entrañas, y como aceite en sus huesos.
Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
19 Séale como vestido con que se cubra, y en lugar de cinto con que se ciña siempre.
Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
20 Este sea el pago de parte de Jehová de los que me calumnian, y de los que hablan mal contra mi alma.
Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
21 Y tú, Jehová Señor, haz conmigo por amor de tu nombre: líbrame, porque tu misericordia es buena.
Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
22 Porque yo estoy afligido y necesitado; y mi corazón está herido dentro de mí.
Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 Voime como la sombra cuando declina; soy sacudido como langosta.
Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
24 Mis rodillas están debilitadas á causa del ayuno, y mi carne desfallecida por falta de gordura.
Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
25 Yo he sido para ellos objeto de oprobio; mirábanme, y meneaban su cabeza.
Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
26 Ayúdame, Jehová Dios mío: sálvame conforme á tu misericordia.
Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
27 Y entiendan que esta es tu mano; [que] tú, Jehová, has hecho esto.
Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
28 Maldigan ellos, y bendice tú: levántense, mas sean avergonzados, y regocíjese tu siervo.
Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
29 Sean vestidos de ignominia los que me calumnian; y sean cubiertos de su confusión como con manto.
Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
30 Yo alabaré á Jehová en gran manera con mi boca, y le loaré en medio de muchos.
Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
31 Porque él se pondrá á la diestra del pobre, para librar su alma de los que le juzgan.
Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.