< Salmos 104 >
1 BENDICE, alma mía, á Jehová. Jehová, Dios mío, mucho te has engrandecido; haste vestido de gloria y de magnificencia.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 El que se cubre de luz como de vestidura, que extiende los cielos como una cortina;
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Que establece sus aposentos entre las aguas; el que pone las nubes por su carroza, el que anda sobre las alas del viento;
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 El que hace á sus ángeles espíritus, sus ministros al fuego flameante.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 El fundó la tierra sobre sus basas; no será jamás removida.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Con el abismo, como con vestido, la cubriste; sobre los montes estaban las aguas.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 A tu reprensión huyeron; al sonido de tu trueno se apresuraron;
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Subieron los montes, descendieron los valles, al lugar que tú les fundaste.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Pusísteles término, el cual no traspasarán; ni volverán á cubrir la tierra.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 [Tú eres] el que envías las fuentes por los arroyos; van entre los montes.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 Abrevan á todas las bestias del campo: quebrantan su sed los asnos montaraces.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Junto á aquellos habitarán las aves de los cielos; entre las ramas dan voces.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 El que riega los montes desde sus aposentos: del fruto de sus obras se sacia la tierra.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 El que hace producir el heno para las bestias, y la hierba para el servicio del hombre; sacando el pan de la tierra.
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 Y el vino que alegra el corazón del hombre, [y] el aceite que hace lucir el rostro, y el pan que sustenta el corazón del hombre.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Llénanse de [jugo] los árboles de Jehová, los cedros del Líbano que él plantó.
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 Allí anidan las aves; en las hayas [hace] su casa la cigüeña.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Los montes altos para las cabras monteses; las peñas, madrigueras para los conejos.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Hizo la luna para los tiempos: el sol conoce su ocaso.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Pone las tinieblas, y es la noche: en ella corretean todas las bestias de la selva.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 Los leoncillos braman á la presa, y para buscar de Dios su comida.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Sale el sol, recógense, y échanse en sus cuevas.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Sale el hombre á su hacienda, y á su labranza hasta la tarde.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 ¡Cuán muchas son tus obras, oh Jehová! Hiciste todas ellas con sabiduría: la tierra está llena de tus beneficios.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 [Asimismo] esta gran mar y ancha de términos: en ella pescados sin número, animales pequeños y grandes.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 Allí andan navíos; allí este leviathán que hiciste para que jugase en ella.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Todos ellos esperan en ti, para que les des su comida á su tiempo.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Les das, recogen; abres tu mano, hártanse de bien.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Escondes tu rostro, túrbanse: les quitas el espíritu, dejan de ser, y tórnanse en su polvo.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Envías tu espíritu, críanse: y renuevas la haz de la tierra.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Sea la gloria de Jehová para siempre; alégrese Jehová en sus obras;
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 El cual mira á la tierra, y ella tiembla; toca los montes, y humean.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 A Jehová cantaré en mi vida: á mi Dios salmearé mientras viviere.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Serme ha suave hablar de él: yo me alegraré en Jehová.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Sean consumidos de la tierra los pecadores, y los impíos dejen de ser. Bendice, alma mía, á Jehová. Aleluya.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.