< Filemón 1 >

1 PABLO, prisionero de Jesucristo, y el hermano Timoteo, á Filemón amado, y coadjutor nuestro;
Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
2 Y á la amada Apphia, y á Archîpo, compañero de nuestra milicia, y á la iglesia [que está] en tu casa:
na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
3 Gracia á vosotros y paz de Dios nuestro Padre, y del Señor Jesucristo.
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
4 Doy gracias á mi Dios, haciendo siempre memoria de ti en mis oraciones.
Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
5 Oyendo tu caridad, y la fe que tienes en el Señor Jesús, y para con todos los santos;
maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
6 Para que la comunicación de tu fe sea eficaz, en el conocimiento de todo el bien que está en vosotros, por Cristo Jesús.
Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
7 Porque tenemos gran gozo y consolación de tu caridad, de que por ti, oh hermano, han sido recreadas las entrañas de los santos.
Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
8 Por lo cual, aunque tengo mucha resolución en Cristo para mandarte lo que conviene,
Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
9 Ruégo[te] más bien por amor, siendo tal cual [soy], Pablo viejo, y aun ahora prisionero de Jesucristo:
Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
10 Ruégote por mi hijo Onésimo, que he engendrado en mis prisiones,
Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
11 El cual en otro tiempo te fué inútil, mas ahora á ti y á mí es útil;
Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
12 El cual te vuelvo á enviar; tú pues, recíbele como á mis entrañas.
Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13 Yo quisiera detenerle conmigo, para que en lugar de ti me sirviese en las prisiones del evangelio;
Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
14 Mas nada quise hacer sin tu consejo, porque tu beneficio no fuese como de necesidad, sino voluntario.
Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
15 Porque acaso por esto se ha apartado de ti por [algún] tiempo, para que le recibieses para siempre; (aiōnios g166)
Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios g166)
16 No ya como siervo, antes más que siervo, [como] hermano amado, mayormente de mí, pero cuánto más de ti, en la carne y en el Señor.
Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
17 Así que, si me tienes por compañero, recíbele como á mí.
Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18 Y si en algo te dañó, ó te debe, ponlo á mi cuenta.
Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
19 Yo Pablo lo escribí de mi mano, yo [lo] pagaré: por no decirte que aun á ti mismo te me debes demás.
Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
20 Sí, hermano, góceme yo de ti en el Señor; recrea mis entrañas en el Señor.
Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
21 Te he escrito confiando en tu obediencia, sabiendo que aun harás más de lo que digo.
Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
22 Y asimismo prepárame también alojamiento; porque espero que por vuestras oraciones os tengo de ser concedido.
Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
23 Te saludan Epafras, mi compañero en la prisión por Cristo Jesús,
Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
24 Marcos, Aristarco, Demas y Lucas, mis cooperadores.
Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
25 La gracia de nuestro Señor Jesucristo sea con vuestro espíritu. Amén. A Filemón fué enviada de Roma por Onésimo, siervo.
Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< Filemón 1 >