< Job 39 >

1 ¿Sabes tú el tiempo en que paren las cabras monteses? ¿ó miraste tú las ciervas cuando están pariendo?
“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
2 ¿Contaste tú los meses de su preñez, y sabes el tiempo cuando han de parir?
Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
3 Encórvanse, hacen salir sus hijos, pasan sus dolores.
Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.
4 Sus hijos están sanos, crecen con el pasto: salen y no vuelven á ellas.
Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
5 ¿Quién echó libre al asno montés, y quién soltó sus ataduras?
“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
6 Al cual yo puse casa en la soledad, y sus moradas en lugares estériles.
Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
7 Búrlase de la multitud de la ciudad: no oye las voces del arriero.
Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
8 Lo oculto de los montes es su pasto, y anda buscando todo lo que está verde.
Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
9 ¿Querrá el unicornio servirte á ti, ni quedar á tu pesebre?
“Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
10 ¿Atarás tú al unicornio con su coyunda para el surco? ¿labrará los valles en pos de ti?
Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
11 ¿Confiarás tú en él, por ser grande su fortaleza, y le fiarás tu labor?
Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
12 ¿Fiarás de él que te tornará tu simiente, y que [la] allegará en tu era?
Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
13 ¿[Diste tú] hermosas alas al pavo real, ó alas y plumas al avestruz?
“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
14 El cual desampara en la tierra sus huevos, y sobre el polvo los calienta,
Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
15 Y olvídase de que los pisará el pie, y que los quebrará bestia del campo.
bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
16 Endurécese para con sus hijos, como si no fuesen suyos, no temiendo que su trabajo haya sido en vano:
Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
17 Porque le privó Dios de sabiduría, y no le dió inteligencia.
kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
18 Luego que se levanta en alto, búrlase del caballo y de su jinete.
Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
19 ¿Diste tú al caballo la fortaleza? ¿vestiste tú su cerviz de relincho?
“Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
20 ¿Le intimidarás tú como á alguna langosta? El resoplido de su nariz es formidable:
Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
21 Escarba la tierra, alégrase en su fuerza, sale al encuentro de las armas:
Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
22 Hace burla del espanto, y no teme, ni vuelve el rostro delante de la espada.
Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
23 Contra él suena la aljaba, el hierro de la lanza y de la pica:
Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
24 Y él con ímpetu y furor escarba la tierra, sin importarle el sonido de la bocina;
Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
25 [Antes como] que dice entre los clarines: ¡Ea!, y desde lejos huele la batalla, el grito de los capitanes, y la vocería.
Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
26 ¿Vuela el gavilán por tu industria, y extiende hacia el mediodía sus alas?
“Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
27 ¿Se remonta el águila por tu mandamiento, y pone en alto su nido?
Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
28 Ella habita y está en la piedra, en la cumbre del peñasco y de la roca.
Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
29 Desde allí acecha la comida: sus ojos observan de muy lejos.
Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
30 Sus pollos chupan la sangre: y donde hubiere cadáveres, allí está.
Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”

< Job 39 >