< Job 38 >
1 Y RESPONDIÓ Jehová á Job desde un torbellino, y dijo:
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 ¿Quién es ése que oscurece el consejo con palabras sin sabiduría?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Ahora ciñe como varón tus lomos; yo te preguntaré, y hazme saber tú.
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 ¿Dónde estabas cuando yo fundaba la tierra? házme[lo] saber, si tienes inteligencia.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 ¿Quién ordenó sus medidas, si lo sabes? ¿ó quién extendió sobre ella cordel?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 ¿Sobre qué están fundadas sus basas? ¿ó quién puso su piedra angular,
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 Cuando las estrellas todas del alba alababan, y se regocijaban todos los hijos de Dios?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 ¿Quién encerró con puertas la mar, cuando se derramaba por fuera [como] saliendo de madre;
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 Cuando puse yo nubes por vestidura suya, y por su faja oscuridad.
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 Y establecí sobre ella mi decreto, y le puse puertas y cerrojo,
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 Y dije: Hasta aquí vendrás, y no pasarás adelante, y ahí parará la hinchazón de tus ondas?
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 ¿Has tú mandado á la mañana en tus días? ¿has mostrado al alba su lugar,
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 Para que ocupe los fines de la tierra, y que sean sacudidos de ella los impíos?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Trasmúdase como lodo bajo de sello, y viene á estar como [con] vestidura:
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 Mas la luz de los impíos es quitada de ellos, y el brazo enaltecido es quebrantado.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 ¿Has entrado tú hasta los profundos de la mar, y has andado escudriñando el abismo?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 ¿Hante sido descubiertas las puertas de la muerte, y has visto las puertas de la sombra de muerte?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 ¿Has tú considerado hasta las anchuras de la tierra? Declara si sabes todo esto.
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 ¿Por dónde va el camino á la habitación de la luz, y dónde está el lugar de las tinieblas?
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 ¿Si llevarás tú [ambas cosas] á sus términos, y entenderás las sendas de su casa?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 ¿Sabíaslo tú porque hubieses ya nacido, ó [porque es] grande el número de tus días?
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 ¿Has tú entrado en los tesoros de la nieve, ó has visto los tesoros del granizo,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 Lo cual tengo yo reservado para el tiempo de angustia, para el día de la guerra y de la batalla?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 ¿Por qué camino se reparte la luz, y se esparce el viento solano sobre la tierra?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 ¿Quién repartió conducto al turbión, y camino á los relámpagos y truenos,
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 Haciendo llover sobre la tierra deshabitada, sobre el desierto, donde no hay hombre,
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 Para hartar la [tierra] desierta é inculta, y para hacer brotar la tierna hierba?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 ¿Tiene la lluvia padre? ¿ó quién engendró las gotas del rocío?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 ¿De qué vientre salió el hielo? y la escarcha del cielo, ¿quién la engendró?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Las aguas se endurecen á manera de piedra, y congélase la haz del abismo.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 ¿Podrás tú impedir las delicias de las Pléyades, ó desatarás las ligaduras del Orión?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 ¿Sacarás tú á su tiempo los signos de los cielos, ó guiarás el Arcturo con sus hijos?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 ¿Supiste tú las ordenanzas de los cielos? ¿dispondrás tú de su potestad en la tierra?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 ¿Alzarás tú á las nubes tu voz, para que te cubra muchedumbre de aguas?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 ¿Enviarás tú los relámpagos, para que ellos vayan? ¿y diránte ellos: Henos aquí?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 ¿Quién puso la sabiduría en el interior? ¿ó quién dió al entendimiento la inteligencia?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 ¿Quién puso por cuenta los cielos con sabiduría? y los odres de los cielos, ¿quién los hace parar,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 Cuando el polvo se ha convertido en dureza, y los terrones se han pegado unos con otros?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 ¿CAZARÁS tú la presa para el león? ¿y saciarás el hambre de los leoncillos,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 Cuando están echados en las cuevas, ó se están en sus guaridas para acechar?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 ¿Quién preparó al cuervo su alimento, cuando sus pollos claman á Dios, bullendo de un lado á otro por carecer de comida?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?