< Job 36 >
2 Espérame un poco, y enseñarte he; porque todavía [tengo] razones en orden á Dios.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 Tomaré mi noticia de lejos, y atribuiré justicia á mi Hacedor.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 Porque de cierto no son mentira mis palabras; contigo [está] el que es íntegro en [sus] conceptos.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 He aquí que Dios es grande, mas no desestima á nadie: es poderoso en fuerza de sabiduría.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 No otorgará vida al impío, y á los afligidos dará su derecho.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 No quitará sus ojos del justo; antes bien con los reyes los pondrá en solio para siempre, y serán ensalzados.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 Y si estuvieren prendidos en grillos, y aprisionados en las cuerdas de aflicción,
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 El les dará á conocer la obra de ellos, y que prevalecieron sus rebeliones.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 Despierta además el oído de ellos para la corrección, y díce[les] que se conviertan de la iniquidad.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 Si oyeren, y [le] sirvieren, acabarán sus días en bien, y sus años en deleites.
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 Mas si no oyeren, serán pasados á cuchillo, y perecerán sin sabiduría.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 Empero los hipócritas de corazón lo irritarán más, y no clamarán cuando él los atare.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 Fallecerá el alma de ellos en su mocedad, y su vida entre los sodomitas.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 Al pobre librará de su pobreza, y en la aflicción despertará su oído.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 Asimismo te apartaría de la boca de la angustia á lugar espacioso, [libre] de todo apuro; y te asentará mesa llena de grosura.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 Mas tú has llenado el juicio del impío, [en vez] de sustentar el juicio y la justicia.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Por lo cual [teme] que [en su] ira no te quite con golpe, el cual no puedas apartar de ti con gran rescate.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 ¿Hará él estima de tus riquezas, ni del oro, ni de todas las fuerzas del poder?
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 No anheles la noche, en que desaparecen los pueblos de su lugar.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Guárdate, no tornes á la iniquidad; pues ésta escogiste más bien que la aflicción.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 He aquí que Dios es excelso con su potencia: ¿qué enseñador semejante á él?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 ¿Quién le ha prescrito su camino? ¿y quién [le] dirá: Iniquidad has hecho?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Acuérdate de engrandecer su obra, la cual contemplan los hombres.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 Los hombres todos la ven; mírala el hombre de lejos.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 He aquí, Dios es grande, y nosotros no le conocemos; ni se puede rastrear el número de sus años.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 El reduce las gotas de las aguas, al derramarse la lluvia según el vapor;
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 Las cuales destilan las nubes, goteando en abundancia sobre los hombres.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 ¿Quién podrá tampoco comprender la extensión de las nubes, y el sonido estrepitoso de su pabellón?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 He aquí que sobre él extiende su luz, y cobija [con ella] las raíces de la mar.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 Bien que por esos medios castiga á los pueblos, á la multitud da comida.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 Con las nubes encubre la luz, y mándale [no brillar], interponiendo [aquéllas].
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 Tocante á ella anunciará [el trueno], su compañero, [que hay] acumulación de ira sobre el que se eleva.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.