< Job 3 >
1 DESPUÉS de esto abrió Job su boca, y maldijo su día.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
3 Perezca el día en que yo nací, y la noche que se dijo: Varón es concebido.
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Sea aquel día sombrío, y Dios no cuide de él desde arriba, ni claridad sobre él resplandezca.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Aféenlo tinieblas y sombra de muerte; repose sobre él nublado, que lo haga horrible como caliginoso día.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 Ocupe la oscuridad aquella noche; no sea contada entre los días del año, ni venga en el número de los meses.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 ¡Oh si fuere aquella noche solitaria, que no viniera canción alguna en ella!
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Maldíganla los que maldicen al día, los que se aprestan para levantar su llanto.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Oscurézcanse las estrellas de su alba; espere la luz, y no venga, ni vea los párpados de la mañana:
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 Por cuanto no cerró las puertas del vientre donde yo estaba, ni escondió de mis ojos la miseria.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 ¿Por qué no morí yo desde la matriz, o fuí traspasado en saliendo del vientre?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 ¿Por qué me previnieron las rodillas? ¿y para qué las tetas que mamase?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 Pues que ahora yaciera yo, y reposara; durmiera, y entonces tuviera reposo,
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 Con los reyes y con los consejeros de la tierra, que edifican para sí los desiertos;
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 O con los príncipes que poseían el oro, que henchían sus casas de plata.
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 O ¿por qué no fuí escondido como aborto, como los pequeñitos que nunca vieron luz?
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 Allí los impíos dejan el perturbar, y allí descansan los de cansadas fuerzas.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 Allí asimismo reposan los cautivos; no oyen la voz del exactor.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 Allí están el chico y el grande; y el siervo libre de su señor.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 ¿Por qué se da luz al trabajado, y vida á los de ánimo en amargura,
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 Que esperan la muerte, y ella no llega, aunque la buscan más que tesoros;
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Que se alegran sobremanera, y se gozan, cuando hallan el sepulcro?
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 ¿[Por qué] al hombre que no sabe por donde vaya, y al cual Dios ha encerrado?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 Pues antes que mi pan viene mi suspiro; y mis gemidos corren como aguas.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 Porque el temor que me espantaba me ha venido, y hame acontecido lo que temía.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 No he tenido paz, no me aseguré, ni me estuve reposado; vínome no obstante turbación.
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”