< Job 15 >

1 Y RESPONDIÓ Eliphaz Temanita, y dijo:
Ndipo Elifazi Mtemani alijibu na kusema,
2 ¿Si proferirá el sabio vana sabiduría, y henchirá su vientre de viento solano?
Mtu mwenye hekima anapaswa kujibu kwa maarifa yasiyofaa na kujijaza mwenyewe na upepo wa mashariki?
3 ¿Disputará con palabras inútiles, y con razones sin provecho?
Anapaswa kuhojiana na mazungumzo yasiyo na faida au na hotuba ambazo kwa hizo yeye hawezi kufanya mema?
4 Tú también disipas el temor, y menoscabas la oración delante de Dios.
Dhahiri, wewe wafifisha heshima ya Mungu; Wewe wazuia heshima kwa yeye,
5 Porque tu boca declaró tu iniquidad, pues has escogido el hablar de los astutos.
kwa maana uovu wako hufundisha midomo yako; Wewe wachagua kuwa na ulimi wa mtu mwenye hila.
6 Tu boca te condenará, y no yo; y tus labios testificarán contra ti.
Mdomo wako mwenyewe hukukukumu wewe, siyo wangu; hakika, midomo yako mwenyewe hushuhudia dhidi yako wewe.
7 ¿Naciste tú primero que Adam? ¿ó fuiste formado antes que los collados?
Je, wewe ni mwanadamu wa kwanza ambaye aliyezaliwa? Wewe ulikuwepo kabla ya vilima kuwepo?
8 ¿Oíste tú el secreto de Dios, que detienes en ti solo la sabiduría?
Wewe Umewahi kusikia maarifa ya siri ya Mungu? Je, wewe wajihesabia mwenye hekima wewe mwenyewe?
9 ¿Qué sabes tú que no sepamos? ¿qué entiendes que no se halle en nosotros?
Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho sisi hatukijui? Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho hakiko katika sisi?
10 Entre nosotros también hay cano, también hay viejo mucho mayor en días que tu padre.
Pamoja nasi wapo pia wenye mvi na watu wazee sana ambao ni wazee zaidi kuliko baba yako.
11 ¿En tan poco tienes las consolaciones de Dios? ¿tienes acaso alguna cosa oculta cerca de ti?
Je, faraja ya Mungu ni ndogo sana kwako, maneno ambayo ni ya upole dhidi yako wewe?
12 ¿Por qué te enajena tu corazón, y por qué guiñan tus ojos,
Kwa nini moyo wako wewe unakupeleka mbali? Kwa nini macho yako yananga'ra,
13 Pues haces frente á Dios con tu espíritu, y sacas [tales] palabras de tu boca?
ili ya kwamba kuirejesha roho yako kwa Mungu na kuyatoa maneno hayo kutoka katika mdomo wako?
14 ¿Qué cosa es el hombre para que sea limpio, y que se justifique el nacido de mujer?
Je, mwanadamu yeye ni nini kwamba yeye anapaswa kuwa safi? Yeye mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke ni nini kwamba yeye anapaswa awe mwenye haki?
15 He aquí que en sus santos no confía, y ni los cielos son limpios delante de sus ojos:
Tazama, Mungu haweki tumaini lake hata kwa mmoja wake aliye mtakatifu; Hakika, mbingu haziko safi machoni pake yeye;
16 ¿Cuánto menos el hombre abominable y vil, que bebe la iniquidad como agua?
jinsi gani asivyo safi ni mmoja aliye mbaya na mla rushwa, mtu ambaye hunywa uovu kama maji!
17 Escúchame; yo te mostraré y te contaré lo que he visto:
Mimi nitakuonyesha wewe; Nisikilize mimi; Mimi nitakutangazia wewe vitu ambavyo nimeviona,
18 (Lo que los sabios nos contaron de sus padres, y no lo encubrieron;
vitu ambavyo watu wenye hekima wamepita chini yake kutoka kwa baba zao, vile vitu ambavyo mababu zao hawakuvificha.
19 A los cuales solos fué dada la tierra, y no pasó extraño por medio de ellos: )
Hawa walikuwa mababu zao, ambao kwao pekee nchi walipewa, na miongoni mwao hakuna mgeni aliyepita.
20 Todos los días del impío, él es atormentado de dolor, y el número de años es escondido al violento.
Mtu mwovu hupitia katika maumivu siku zake zote, idadi ya miaka iliyowekwa juu kwa mtesaji kuteseka.
21 Estruendos espantosos hay en sus oídos; en la paz le vendrá quien lo asuele.
Sauti ya vitisho katika masikio yake; pindi yeye yuko katika kufanikiwa, mharibu atakuja juu yake yeye.
22 El no creerá que ha de volver de las tinieblas, y está mirando al cuchillo.
Yeye hafikiri kwamba yeye atarudi kutoka katika giza; Upanga humngojea yeye.
23 Desasosegado á comer siempre, sabe que le está aparejado día de tinieblas.
Yeye huenda sehemu mbali mbali kwa ajili ya mkate, akisema, 'Kiko wapi? ' Yeye anatambua kuwa siku ya giza iko mkononi.
24 Tribulación y angustia le asombrarán, y esforzaránse contra él como un rey apercibido para la batalla.
Dhiki na mateso makali humfanya aogope; wao hushinda dhidi yake yeye, kama mfalme tayari kwa vita.
25 Por cuanto él extendió su mano contra Dios, y se esforzó contra el Todopoderoso,
Kwa sababu yeye ameunyosha mkono wake dhidi ya Mungu na ameishi kwa kiburi dhidi ya aliye mkuu,
26 El le acometerá en la cerviz, en lo grueso de las hombreras de sus escudos:
huyu mtu mwovu hukimbia kwa Mungu na shingo ngumu, kwa vifundo vikubwa vya ngao.
27 Porque cubrió su rostro con su gordura, é hizo pliegues sobre los ijares;
Hii ni kweli, hata ingawa yeye amefunika uso wake kwa mafuta yake na amekusanya mafuta juu ya viuno vyake,
28 Y habitó las ciudades asoladas, las casas inhabitadas, que estaban puestas en montones.
na ameishi katika miji yenye ukiwa; katika nyumba ambazo hakuna mwanadamu anayeishi humo sasa na ambazo zilikuwa tayari kuwa magofu.
29 No enriquecerá, ni será firme su potencia, ni extenderá por la tierra su hermosura.
Yeye hatakuwa tajiri; utajiri wake yeye hautadumu; hata kivuli chake hakitadumu katika nchi.
30 No se escapará de las tinieblas: la llama secará sus ramos, y con el aliento de su boca perecerá.
Yeye hatatoka nje ya giza; mwali wa moto utakausha matawi yake; katika pumzi ya kinywa cha Mungu yeye ataenda zake.
31 No confíe el iluso en la vanidad; porque ella será su recompensa.
Mwacheni yeye asitumaini katika vitu visivyofanya kazi, akijidanganya yeye mwenyewe; maana upuuzi utakuwa mshahara wake yeye.
32 El será cortado antes de su tiempo, y sus renuevos no reverdecerán.
Itatokea kabla ya wakati wake yeye atapaswa kufa; tawi lake halitakuwa kijani.
33 El perderá su agraz como la vid, y derramará su flor como la oliva.
Yeye atazipukutisha zabibu zake zisizovunwa kama mzabibu; yeye atayaondoa maua yake kama mti wa mzeituni.
34 Porque la sociedad de los hipócritas será asolada, y fuego consumirá las tiendas de soborno.
Kwa maana msaada wa watu wasiomcha Mungu utakuwa tasa; moto utateketeza hema za rushwa.
35 Concibieron dolor, y parieron iniquidad; y las entrañas de ellos meditan engaño.
Wao wanabeba mimba yenye ubaya na kuzaa uovu; tumbo lao hutunga mimba ya udanganifu.

< Job 15 >