< Job 11 >

1 Y RESPONDIÓ Sophar Naamathita, y dijo:
Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
2 ¿Las muchas palabras no han de tener respuesta? ¿y el hombre parlero será justificado?
“Je, maneno haya yote yapite bila kujibiwa? Je, huyu mnenaji athibitishwe kuwa na haki?
3 ¿Harán tus falacias callar á los hombres? ¿y harás escarnio, y no habrá quien te avergüence?
Je, maneno yako ya upuzi yawafanye watu wanyamaze kimya? Je, mtu asikukemee unapofanya dhihaka?
4 Tú dices: Mi conversar es puro, y yo soy limpio delante de tus ojos.
Unamwambia Mungu, ‘Imani yangu ni kamili nami ni safi mbele zako.’
5 Mas ¡oh quién diera que Dios hablara, y abriera sus labios contigo,
Aha! Laiti kwamba Mungu angesema, kwamba angefungua midomo yake dhidi yako,
6 Y que te declarara los arcanos de la sabiduría, que [son] de doble [valor] que la hacienda! Conocerías entonces que Dios te ha castigado menos que tu iniquidad merece.
naye akufunulie siri za hekima, kwa kuwa hekima ya kweli ina pande mbili. Ujue hili: Mungu amesahau hata baadhi ya dhambi zako.
7 ¿Alcanzarás tú el rastro de Dios? ¿llegarás tú á la perfección del Todopoderoso?
“Je, waweza kujua siri za Mungu? Je, waweza kuyachunguza mambo yote kumhusu Mwenyezi?
8 Es más alto que los cielos: ¿qué harás? Es más profundo que el infierno: ¿cómo lo conocerás? (Sheol h7585)
Ni juu mno kuliko mbingu: waweza kufanya nini? Kina chake ni kirefu kuliko kuzimu: wewe waweza kujua nini? (Sheol h7585)
9 Su dimensión es más larga que la tierra, y más ancha que la mar.
Kipimo chake ni kirefu kuliko dunia, nacho ni kipana kuliko bahari.
10 Si cortare, ó encerrare, ó juntare, ¿quién podrá contrarrestarle?
“Kama akija na kukufunga gerezani, na kuitisha mahakama, ni nani awezaye kumpinga?
11 Porque él conoce á los hombres vanos: ve asimismo la iniquidad, ¿y no hará caso?
Hakika anawatambua watu wadanganyifu; naye aonapo uovu, je, haangalii?
12 El hombre vano se hará entendido, aunque nazca como el pollino del asno montés.
Mpumbavu aweza kuwa mwenye hekima, endapo mtoto wa punda-mwitu atazaliwa mwanadamu.
13 Si tú apercibieres tu corazón, y extendieres á él tus manos;
“Hata sasa ukiutoa moyo wako kwake na kumwinulia mikono yako,
14 Si alguna iniquidad hubiere en tu mano, y la echares de ti, y no consintieres que more maldad en tus habitaciones;
ukiiondolea mbali ile dhambi iliyo mkononi mwako wala usiuruhusu uovu ukae hemani mwako,
15 Entonces levantarás tu rostro limpio de mancha, y serás fuerte y no temerás:
ndipo utainua uso wako bila aibu; utasimama imara bila hofu.
16 Y olvidarás tu trabajo, ó te acordarás de él como de aguas que pasaron:
Hakika utaisahau taabu yako, utaikumbuka tu kama maji yaliyokwisha kupita.
17 Y en mitad de la siesta se levantará bonanza; resplandecerás, y serás como la mañana:
Maisha yako yatangʼaa kuliko adhuhuri, nalo giza litakuwa kama alfajiri.
18 Y confiarás, que habrá esperanza; y cavarás, y dormirás seguro:
Utakuwa salama, kwa kuwa lipo tumaini; utatazama pande zote na kupumzika kwa salama.
19 Y te acostarás, y no habrá quien te espante: y muchos te rogarán.
Utalala, wala hakuna atakayekuogofya, naam, wengi watajipendekeza kwako.
20 Mas los ojos de los malos se consumirán, y no tendrán refugio; y su esperanza será agonía del alma.
Bali macho ya waovu hayataona, wokovu utawaepuka; tarajio lao litakuwa ni hangaiko la mtu anayekata roho.”

< Job 11 >