< Salmos 96 >

1 Cantád a Jehová canción nueva: cantád a Jehová toda la tierra.
Oh, mwimbieni Yahwe wimbo mpya; mwimbieni Yahwe, nchi yote.
2 Cantád a Jehová, bendecíd su nombre: anunciád de día en día su salud.
Mwimbieni Yahwe, tukuzeni jina lake; tangazeni wokovu wake siku hadi siku.
3 Contád en las naciones su gloria: en todos los pueblos sus maravillas.
Tangazeni utukufu wake kati ya mataifa, matendo yake ya ajabu kati ya mataifa.
4 Porque grande es Jehová, y muy alabado: terrible sobre todos los dioses.
Maana Yahwe ni mkuu na wakusifiwa sana. Ni wakuhofiwa kuliko miungu mingine.
5 Porque todos los dioses de los pueblos son ídolos: mas Jehová hizo los cielos.
Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
6 Alabanza y gloria está delante de él: fortaleza y gloria está en su santuario.
Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
7 Dad a Jehová, o! familias de los pueblos, dad a Jehová la gloria y la fortaleza.
Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
8 Dad a Jehová la honra de su nombre: tomád presentes, y veníd a sus patios.
Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.
9 Encorváos a Jehová en la hermosura de su santuario: teméd delante de él toda la tierra.
Mpigieni magoti Yahwe mkiwa mmevaa mavazi ambayo yanaheshimu utakatifu wake. Nchi yote tetemekeni mbele zake.
10 Decíd en las naciones: Jehová reinó, también compuso el mundo, no se meneará: juzgará a los pueblos en justicia.
Semeni kati ya mataifa, Yahwe anatawala.” Ulimwengu pia umeimarishwa; hauwezi kutikiswa. Yeye huwahukumu watu kwa haki.
11 Alégrense los cielos, y regocíjese la tierra: brame la mar y su plenitud.
Mbingu na zifurahi, na nchi ishangilie; bahari na ivume na vyote viijazavyo vipige kelele kwa shangwe.
12 Regocíjese el campo y todo lo que en él está: entonces exultarán todos los árboles de la breña,
Mashamba yashangilie na vyote vilivyomo. Kisha miti ya mstuni ipige kelele kwa furaha
13 Delante de Jehová que vino: porque vino a juzgar la tierra. Juzgará al mundo con justicia, y a los pueblos con su verdad.
mbele za Yahwe, maana yeye anakuja. Anakuja kuihukumu nchi. Naye atauhukumu ulumwengu kwa haki na mataifa kwa uaminifu wake.

< Salmos 96 >