< Salmos 96 >
1 Cantád a Jehová canción nueva: cantád a Jehová toda la tierra.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 Cantád a Jehová, bendecíd su nombre: anunciád de día en día su salud.
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Contád en las naciones su gloria: en todos los pueblos sus maravillas.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 Porque grande es Jehová, y muy alabado: terrible sobre todos los dioses.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 Porque todos los dioses de los pueblos son ídolos: mas Jehová hizo los cielos.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 Alabanza y gloria está delante de él: fortaleza y gloria está en su santuario.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Dad a Jehová, o! familias de los pueblos, dad a Jehová la gloria y la fortaleza.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 Dad a Jehová la honra de su nombre: tomád presentes, y veníd a sus patios.
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 Encorváos a Jehová en la hermosura de su santuario: teméd delante de él toda la tierra.
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Decíd en las naciones: Jehová reinó, también compuso el mundo, no se meneará: juzgará a los pueblos en justicia.
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Alégrense los cielos, y regocíjese la tierra: brame la mar y su plenitud.
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 Regocíjese el campo y todo lo que en él está: entonces exultarán todos los árboles de la breña,
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 Delante de Jehová que vino: porque vino a juzgar la tierra. Juzgará al mundo con justicia, y a los pueblos con su verdad.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.