< Salmos 94 >
1 Dios de venganzas Jehová, Dios de venganzas, muéstrate.
Ee Bwana, ulipizaye kisasi, Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.
2 Ensálzate, o! Juez de la tierra: da el pago a los soberbios.
Ee Mhukumu wa dunia, inuka, uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.
3 ¿Hasta cuándo los impíos, o! Jehová, hasta cuándo los impíos se regocijarán?
Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
4 ¿Pronunciarán, hablarán cosas duras? ¿ensalzarse han todos los que obran iniquidad?
Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
5 A tu pueblo, o! Jehová, quebrantan, y a tu heredad afligen.
Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
6 A la viuda y al extranjero matan, y a los huérfanos quitan la vida.
Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.
7 Y dijeron: No verá Jehová: y, no entenderá el Dios de Jacob.
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
8 Entendéd necios en el pueblo: y vosotros insensatos, ¿cuándo seréis sabios?
Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?
9 ¿El que plantó la oreja, no oirá? ¿él que formó el ojo, no verá?
Je, aliyeweka sikio asisikie? Aliyeumba jicho asione?
10 ¿El que castiga a las gentes, no reprenderá? ¿el que enseña al hombre la ciencia?
Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?
11 Jehová conoce los pensamientos de los hombres: que son vanidad.
Bwana anajua mawazo ya mwanadamu; anajua kwamba ni ubatili.
12 Bienaventurado el varón a quien tú Jehová, castigares, y en tu ley le enseñares.
Ee Bwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, mtu unayemfundisha kwa sheria yako,
13 Para hacerle quieto en los días de aflicción, entre tanto que se cava el hoyo para el impío.
unampa utulivu siku za shida, mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya mwovu.
14 Porque no dejará Jehová a su pueblo, ni desamparará a su heredad.
Kwa kuwa Bwana hatawakataa watu wake, hatauacha urithi wake.
15 Porque el juicio será vuelto hasta justicia, y en pos de ella irán todos los rectos de corazón.
Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki, wote walio na mioyo minyofu wataifuata.
16 ¿Quién se levanta por mí contra los malignos? ¿Quién está por mí contra los que obran iniquidad?
Ni nani atakayeinuka dhidi ya mwovu kwa ajili yangu? Ni nani atakayenikinga dhidi ya watenda maovu?
17 Si no me ayudara Jehová, presto morara mi alma con los muertos.
Kama Bwana asingelinisaidia upesi, ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo.
18 Mas si decía: Mi pie resbala, tu misericordia, o! Jehová, me sustentaba.
Niliposema, “Mguu wangu unateleza,” Ee Bwana, upendo wako ulinishikilia.
19 En la multitud de mis pensamientos dentro de mí, tus consolaciones alegraban mi alma.
Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu, faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu.
20 ¿Juntarse ha contigo el trono de iniquidades, que cria agravio en el mandamiento?
Je, kiti cha utawala wa udhalimu kitajiunga nawe, ule utawala uletao taabu kutokana na sheria zake?
21 Pónense en ejército contra la vida del justo: y condenan la sangre inocente.
Huungana kuwashambulia wenye haki, kuwahukumu kufa wasio na hatia.
22 Mas Jehová me ha sido por refugio: y mí Dios por peña de mi confianza.
Lakini Bwana amekuwa ngome yangu, na Mungu wangu amekuwa mwamba ninaoukimbilia.
23 El cual hizo volver contra ellos su iniquidad: y con su maldad los talará: talarlos ha Jehová nuestro Dios.
Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao; Bwana Mungu wetu atawaangamiza.