< Salmos 91 >

1 El que habita en el escondedero del Altísimo, morará en la sombra del Omnipotente.
Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
2 Diré a Jehová: Esperanza mía y castillo mío: Dios mío: asegurarme he en él.
Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
3 Porque él te escapará del lazo del cazador: de la mortandad de destrucciones.
Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
4 Con su ala te cubrirá, y debajo de sus alas estarás seguro: escudo y adarga, es su verdad.
Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
5 No habrás temor de espanto nocturno, ni de saeta que vuele de día,
Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6 Ni de pestilencia que ande en oscuridad: ni de mortandad que destruya al mediodía.
wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7 Caerán a tu lado mil, y diez mil a tu diestra: a ti no llegará.
Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8 Ciertamente con tus ojos mirarás; y verás la recompensa de los impíos.
Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9 Porque tú, o! Jehová, eres mi esperanza: y al Altísimo has puesto por tu habitación.
Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
10 No se ordenará para ti mal: ni plaga tocará a tu morada.
Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
11 Porque a sus ángeles mandará cerca de ti, que te guarden en todos tus caminos.
Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
12 En las manos te llevarán, porque tu pie no tropiece en piedra.
Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
13 Sobre el león y el basilisco pisarás, hollarás al cachorro del león, y al dragón.
Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
14 Por cuanto en mí ha puesto su voluntad, yo también le escaparé: ponerle he alto, por cuanto ha conocido mi nombre.
Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
15 Llamarme ha, y yo le responderé: con él estaré yo en la angustia: escaparle he, y glorificarle he.
Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
16 De longura de días le hartaré: y mostrarle he mi salud.
Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.

< Salmos 91 >