< Salmos 75 >
1 Alabarte hemos, o! Dios, alabar te hemos; que cercano está tu nombre: cuenten todos tus maravillas.
Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
2 Cuando yo tuviere tiempo, yo juzgaré rectamente.
Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
3 La tierra se arruinaba, y sus moradores: yo compuse sus columnas. (Selah)
Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
4 Dije a los malvados: No os enloquezcáis: y a los impíos: No alcéis el cuerno.
Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
5 No levantéis en alto vuestro cuerno; no habléis con cerviz gruesa.
Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
6 Porque ni de oriente, ni de occidente, ni del desierto viene el ensalzamiento.
Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
7 Porque Dios, que es el juez; a este abate, y a aquel ensalza.
Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
8 Que el cáliz está en la mano de Jehová, y lleno de vino bermejo de mistura, y él derrama de aquí: ciertamente sus heces chuparán, y beberán todos los impíos de la tierra.
Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
9 Y yo anunciaré siempre: cantaré alabanzas al Dios de Jacob.
Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
10 Y quebraré todos los cuernos de los pecadores: y los cuernos del justo serán ensalzados.
Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”