< Salmos 71 >

1 En ti, Jehová, he esperado; no sea yo confundido para siempre.
Katika wewe, Yahwe, napatakimbilio salama; usiniache niaibishwe.
2 Escápame, y líbrame en tu justicia: inclina a mí tu oído, y sálvame.
Uniokoe na kunifanya salama katika haki yako; geuzia sikio lako kwangu.
3 Séme por peña de fortaleza donde venga continuamente: mandado has que yo sea salvo, porque tú eres mi roca y mi castillo.
Uwe kwagu mwamba kwa ajili ya kimbilio salama ambako naweza kwenda siku zote; wewe umeamuru kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4 Dios mío, escápame de la mano del impío, de la mano del perverso y falsario.
Uniokoe mimi, Mungu wangu, kutoka katika mkono wa asiye haki na katili.
5 Porque tú eres mi esperanza, Señor Jehová: seguridad mía desde mi mocedad.
Maana wewe ni tumaini langu, Bwana Yahwe. Nimekuamini wewe siku zote tangu nilipokuwa mtoto.
6 Por ti he sido sustentado desde el vientre: de las entrañas de mi madre tú fuiste el que me sacaste: de ti ha sido siempre mi alabanza.
Nimekuwa nikisaidiwa na wewe tangu tumboni; wewe ndiye yule uliyenitoa tumboni mwa mama yangu; sifa zangu zitakuhusu wewe siku zote.
7 Como prodigio he sido a muchos; y tú mi refugio fuerte.
Mimi ni mfano bora kwa watu wangu; wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.
8 Sea llena mi boca de tu alabanza, todo el día de tu gloria.
Mama yangu atajawa na sifa zako, siku zote akikuheshimu.
9 No me deseches en el tiempo de la vejez: cuando mi fuerza se acabare, no me desampares.
Usinitupe katika siku za miaka ya uzee wangu; usiniache wakati nguvu zangu zitakapoisha.
10 Porque mis enemigos han dicho de mí; y los que asechan mi vida, consultaron juntamente,
Maana adui zangu wanazungumza kuhusu mimi; wale wanao fatilia uhai wangu wanapanga njama pamoja.
11 Diciendo: Dios le ha dejado: perseguíd, y tomádle, porque no hay quien le libre.
Wao husema, “Mungu amemuacha; mfuateni na mumchukue, maana hakuna yeyote awezaye kumuokoa yeye.”
12 O! Dios, no te alejes de mí: Dios mío, apresúrate para ayudarme.
Mungu, usiwe mbali nami; Mungu wangu, harakisha kunisaidia mimi.
13 Sean avergonzados, perezcan, los adversarios de mi alma: sean cubiertos de vergüenza y de confusión, los que buscan mi mal.
Waaibishwe na kuharibiwa, wale walio adui wa uhai wangu; wavishwe laumu na kudharauliwa, wale watafutao kuniumiza.
14 Y yo siempre esperaré: y añadiré sobre toda tu alabanza.
Lakini nitakutumainia wewe siku zote na nitakusifu wewe zaidi na zaidi.
15 Mi boca recontará tu justicia: todo el día tu salud, aunque no sé el número.
Kinywa changu kitaongea kuhusu haki yako na wokovu wako mchana kutwa, ingawa ziwezi kuzielewa maana ni nyingi mno.
16 Vendré a las valentías del Señor Jehová: haré memoria de la justicia de ti solo.
Nitakuja na matendo yenye nguvu ya Bwana Yahwe; nitataja haki yako, yako pekee.
17 O! Dios, enseñásteme desde mi mocedad, y hasta ahora: manifestaré tus maravillas.
Mungu, tangu ujana wangu wewe umenifundisha; hata sasa ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18 Y aun hasta la vejez y las canas: o! Dios, no me desampares: hasta que denuncie tu brazo a la posteridad: tus valentías a todos los que vendrán.
Hakika, hata niwapo mzee na mvi kichwani, Mungu, usiniache mimi, kama ambavyo nimekuwa nikitanga nguvu yako kwa vizazi vijavyo, na uweza wako kwa yeyote ajaye.
19 Y tu justicia, o! Dios, hasta lo alto: porque has hecho grandes cosas: o! Dios, ¿quién como tú?
Pia haki yako, Mungu, iko juu sana; wewe ambaye umefanya mambo makuu, Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20 Que me has hecho ver muchas angustias y males: volverás, y darme has vida: y de los abismos de la tierra volverás a levantarme.
Wewe ambaye umetuonesha sisi mateso mengi utatuhuisha tena na utatupandisha tena juu kutoka kwenye kina cha nchi.
21 Aumentarás mí magnificencia: y volverás a consolarme.
Uiongeze heshima yangu; rudi tena na unifariji.
22 Asimismo yo te alabaré con instrumento de salterio: tu verdad, o! Dios mío, cantaré a ti en la arpa, o! Santo de Israel.
Nami pia nitakushukuru kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako, Mungu wangu; kwako nitaimba sifa kwa kinubi, Mtakatifu wa Israel.
23 Mis labios cantarán cuando salmeare a ti: y mi alma, a la cual redimiste.
Midomo yangu itapiga kelele kwa sababu ya furaha wakati nikikuimbia sifa, hata kwa roho yangu, ambayo wewe umeikomboa.
24 Asimismo mi lengua todo el día hablará de tu justicia: por cuanto fueron avergonzados, por cuanto fueron confusos, los que procuraban mi mal.
Ulimi wangu pia utaongea kuhusu haki yangu mchana kutwa; maana wameaibishwa na kuvurugwa, wale waliotafuta kuniumiza.

< Salmos 71 >