< Salmos 143 >

1 Jehová, oye mi oración, escucha mis ruegos por tu verdad: respóndeme por tu justicia.
Ee Yahwe, usikie maombi yangu; sikia kuomba kwangu. Kwa sababu ya uaminifu wa agano lako na haki yako, unijibu!
2 Y no entres en juicio con tu siervo; porque no se justificará delante de ti ningún viviente.
Usimuhukumu mtumishi wako, kwa kuwa machoni pako hamna aliye haki.
3 Porque ha perseguido el enemigo mi alma: ha quebrantado a tierra mi vida: me ha hecho habitar en tinieblas como los ya muertos.
Adui ameifuatia nafsi yangu; amenisukuma hadi chini; amenifanya niishi gizani kama wale ambao wamekwisha kufa siku nyingi zilizopita.
4 Y mi espíritu se angustió dentro de mí: mi corazón se pasmó.
Na roho yangu inazidiwa ndani yangu; moyo wangu unakata tamaa.
5 Acordéme de los días antiguos: meditaba en todas tus obras: meditaba en las obras de tus manos.
Nakumbuka siku za zamani zilizopita; nayatafakari matendo yako yote; nawaza juu ya utimilifu wako.
6 Extendí mis manos a ti: mi alma, como la tierra sedienta, a ti. (Selah)
Nakunyoshea mikono yangu katika maombi; nafsi yangu inakuonea kiu katika nchi kavu. (Selah)
7 Respóndeme presto, o! Jehová, que desmaya mi espíritu: no escondas de mí tu rostro, y sea semejante a los que descienden a la sepultura.
Unijibu upesi, Yahwe, kwa sababu roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, vinginevyo nitakuwa kama wale waendao chini shimoni.
8 Házme oír por la mañana tu misericordia, porque en ti he confiado: házme saber el camino por donde ande, porque a ti he alzado mi alma.
Unifanye kusikia uaminifu wa agano lako wakati wa asubuhi, maana ninakuamini wewe. Unionyeshe njia niipasayo kutembea kwayo, kwa maana nakuinulia wewe nafsi yangu.
9 Escápame de mis enemigos, o! Jehová: a ti me acojo.
Uniokoe dhidi ya adui zangu, Yahwe; nakimbilia kwako ili nijifiche.
10 Enséñame a hacer tu voluntad, porque tú eres mi Dios. Tu buen Espíritu me guie a tierra de rectitud.
Unifundishe kufanya mapenzi yako, maana wewe ni Mungu wangu. Roho wako mwema na aniongoze mimi katika nchi ya unyoofu.
11 Por tu nombre, o! Jehová, me vivificarás; por tu justicia sacarás mi alma de angustia.
Ee Yahwe, kwa ajili ya jina lako, unihifadhi hai; katika haki yako uitoe nafsi yangu taabuni.
12 Y por tu misericordia disiparás mis enemigos, y destruirás todos los adversarios de mi alma; porque yo soy tu siervo.
Katika uaminifu wa agano lako uwaondoshe maadui zangu na uwaangamize maadui wa uhai wangu, maana mimi ni mtumishi wako.

< Salmos 143 >