< Salmos 121 >
1 Alzaré mis ojos a los montes de donde vendrá mi socorro.
Nitayainua macho yangu nitazame milimani. Msaada wangu utatoka wapi?
2 Mi socorro es de parte de Jehová; que hizo los cielos y la tierra.
Msaada wangu unatoka kwa Yahwe, aliyezifanya mbingu na nchi.
3 No dará tu pie al resbaladero: ni se dormirá el que te guarda.
Hatauacha mguu wako uteleze; yeye akulindaye hatasinzia.
4 He aquí, no se adormecerá, ni dormirá el que guarda a Israel.
Tazama, mlinzi wa Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi kamwe.
5 Jehová será tu guardador: Jehová será tu sombra sobre tu mano derecha.
Yahwe ni mlinzi wako; Yahwe ni uvuli mkono wako wa kuume.
6 De día el sol no te fatigará, ni la luna de noche.
Jua halitakudhuru wakati wa mchana, wala mwezi wakati wa usiku.
7 Jehová te guardará de todo mal; él guardará a tu alma.
Yahwe atakulinda na madhara yote, na ataulinda uhai wako.
8 Jehová guardará tu salida, y tu entrada, desde ahora y hasta siempre.
Yahwe atakulinda katika yote ufanyayo sasa na hata milele.