< Salmos 111 >

1 Alabaré a Jehová con todo el corazón, en la compañía y congregación de los rectos.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Grandes son las obras de Jehová: buscadas de todos los que las quieren.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Honra y hermosura es su obra; y su justicia permanece para siempre.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 Hizo memorables sus maravillas: clemente y misericordioso es Jehová.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 Dio mantenimiento a los que le temen: para siempre se acordará de su concierto.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 La fortaleza de sus obras anunció a su pueblo: dándoles la heredad de los Gentiles.
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 Las obras de sus manos son verdad y juicio: fieles son todos sus mandamientos;
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 Afirmados por siglo de siglo: hechos en verdad y en rectitud.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 Redención ha enviado a su pueblo; ordenó para siempre su concierto: santo y terrible es su nombre.
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 El principio de la sabiduría es el temor de Jehová; entendimiento bueno es a todos los que guardan sus mandamientos: su loor permanece para siempre.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Salmos 111 >