< Salmos 106 >

1 Alabád a Jehová, porque es bueno: porque para siempre es su misericordia.
Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 ¿Quién dirá las valentías de Jehová? ¿ quién contará sus alabanzas?
Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
3 Dichosos los que guardan juicio, los que hacen justicia en todo tiempo.
Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
4 Acuérdate de mí, o! Jehová, en la voluntad de tu pueblo: visítame con tu salud;
Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
5 Para que yo vea el bien de tus escogidos: para que me alegre en la alegría de tu gente: y me gloríe con tu heredad.
Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
6 Pecamos con nuestros padres, hicimos iniquidad, hicimos impiedad.
Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
7 Nuestros padres en Egipto no entendieron tus maravillas: no se acordaron de la muchedumbre de tus misericordias: mas se rebelaron sobre la mar, en el mar Bermejo.
Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
8 Y salvólos por su nombre: para hacer notoria su fortaleza.
Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
9 Y reprendió al mar Bermejo, y secóse: e hízolos ir por el abismo, como por un desierto.
Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
10 Y salvólos de mano del enemigo: y rescatólos de mano del adversario.
Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
11 Y cubrieron las aguas a sus enemigos: uno de ellos no quedó.
Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
12 Y creyeron a sus palabras: y cantaron su alabanza.
Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
13 Apresuráronse, olvidáronse de sus obras: no esperaron en su consejo.
Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
14 Y desearon mal deseo en el desierto: y tentaron a Dios en la soledad.
Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
15 Y él les dio lo que pidieron: y envió flaqueza en sus almas.
Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
16 Y tomaron zelo contra Moisés en el campo: contra Aarón santo de Jehová.
Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
17 Abrióse la tierra, y tragó a Datán, y cubrió a la compañía de Abirom.
Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
18 Y encendióse el fuego en su compañía: la llama quemó a los impíos.
Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
19 Hicieron el becerro en Horeb: y encorváronse a un vaciadizo.
Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
20 Y trocaron su gloria por la imagen de un buey, que come yerba.
Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
21 Olvidaron al Dios de su salud: que había hecho grandezas en Egipto,
Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
22 Maravillas en la tierra de Cam, temerosas cosas sobre el mar Bermejo.
Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
23 Y trató de destruirlos, si Moisés su escogido no se pusiera al portillo delante de él: para apartar su ira para que no los destruyese.
Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
24 Y aborrecieron la tierra deseable: no creyeron a su palabra.
Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
25 Y murmuraron en sus tiendas; y no oyeron la voz de Jehová.
bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
26 Y alzó su mano para ellos; para postrarlos en el desierto,
Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
27 Y para postrar su simiente entre las naciones; y esparcirlos por las tierras.
akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
28 Y allegáronse a Baal-pehor; y comieron los sacrificios de los muertos.
Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
29 Y ensañáron le con sus obras; y aumentó en ellos la mortandad.
Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
30 Y púsose Finees, y juzgó; y la mortandad cesó.
Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
31 Y fuéle contado a justicia de generación a generación para siempre.
Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
32 Y ensañáron le a las aguas de Meriba; e hizo mal a Moisés por causa de ellos.
Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
33 Porque hicieron rebelar a su espíritu, y habló inconsideradamente con sus labios.
Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
34 No destruyeron los pueblos, que Jehová les dijo:
Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
35 Antes se envolvieron con los Gentiles; y aprendieron sus obras:
bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
36 Y sirvieron a sus ídolos: los cuales les fueron por ruina.
nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
37 Y sacrificaron sus hijos y sus hijas a los demonios.
Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
38 Y derramaron la sangre inocente: la sangre de sus hijos y de sus hijas, que sacrificaron a los ídolos de Canaán; y la tierra fue contaminada con sangres.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
39 Y contamináronse con sus obras, y fornicaron con sus hechos.
Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
40 Y encendióse el furor de Jehová sobre su pueblo; y abominó su heredad.
Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
41 Y entrególos en poder de los Gentiles; y enseñoreáronse de ellos los que les aborrecían.
Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
42 Y sus enemigos les oprimieron, y fueron quebrantados debajo de su mano.
Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
43 Muchas veces los escapó, y ellos se rebelaron a su consejo; y fueron humillados por su maldad.
Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
44 Mas él miraba, cuando estaban en angustia, oyendo su clamor.
Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
45 Y acordábase de su concierto con ellos, y arrepentíase conforme a la muchedumbre de sus miseraciones.
Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
46 Y hacía que tuviesen de ellos misericordia todos los que los tenían cautivos.
Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
47 Sálvanos Jehová Dios nuestro, y júntanos de entre las naciones, para que loemos tu santo nombre, para que nos gloriemos de tus alabanzas.
Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
48 Bendito Jehová Dios de Israel desde el siglo y hasta el siglo; y diga todo el pueblo: Amén, Alelu- Jah.
Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.

< Salmos 106 >