< Proverbios 4 >
1 Oíd hijos la enseñanza del padre; y estád atentos, para que sepáis inteligencia.
Wanangu, sikilizeni, fundisho la baba, na zingatieni ili mjue maana ya ufahamu.
2 Porque os doy buen enseñamiento: no desamparéis mi ley.
Mimi ninawapa mafundisho mazuri; msiyaache mafundisho yangu.
3 Porque yo fui hijo de mi padre, delicado y único delante de mi madre:
Mimi nilikuwa mwana kwa baba yangu, mpole na mtoto pekee kwa mama yangu,
4 Y enseñábame, y me decía: Sustente mis razones tu corazón: guarda mis mandamientos, y vivirás.
baba alinifundisha akiniambia, “Moyo wako uzingatie sana maneno yangu; shika amri zangu nawe uishi.
5 Adquiere sabiduría, adquiere inteligencia: no te olvides, ni te apartes de las razones de mi boca.
Jipatie hekima na ufahamu; usisahau na kuyakataa maneno ya kinywa changu;
6 No la dejes, y ella te guardará; ámala, y conservarte ha.
usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
7 Primeramente sabiduría: adquiere sabiduría, y ante toda tu posesión adquiere inteligencia.
Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
8 Engrandécela, y ella te engrandecerá; ella te honrará, cuando tú la hubieres abrazado.
Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
9 Dará a tu cabeza aumento de gracia: corona de hermosura te entregará.
Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
10 Oye, hijo mío, y recibe mis razones; y multiplicársete han años de vida.
Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
11 Por el camino de la sabiduría te he encaminado; y por veredas derechas te he hecho andar.
Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.
12 Cuando por ellas anduvieres, no se estrecharán tus pasos; y si corrieres, no tropezarás.
Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.
13 Ten asida la instrucción, no la dejes: guárdala, porque ella es tu vida.
Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
14 No entres por la vereda de los impíos: ni vayas por el camino de los malos:
Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.
15 Desampárala; no pases por ella: apártate de ella, y pasa.
Jiepushe nayo, usipite katika njia hiyo; geuka na upite njia nyingine.
16 Porque no duermen, si no hicieren mal; y pierden su sueño, si no han hecho caer.
Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
17 Porque comen pan de maldad, y beben vino de robos.
Maana wao hula mkate wa uovu na hunywa divai ya vurugu.
18 Mas la vereda de los justos es como la luz del lucero: auméntase, y alumbra hasta que el día es perfecto.
Bali njia ya mwenye kutenda haki ni kama mwanga ung'aao, huangaza zaidi na zaidi hadi mchana inapowasili kwa ukamilifu.
19 El camino de los impíos es como la oscuridad: no saben en qué tropiezan.
Njia ya waovu ni kama giza - hawajui ni kitu gani huwa wanajikwaa juu yake.
20 Hijo mío, está atento a mis palabras; y a mis razones inclina tu oreja:
Mwanangu, zingatia maneno yangu; sikiliza kauli zangu.
21 No se aparten de tus ojos: mas guárdalas en medio de tu corazón;
Usiziache zikaondoka machoni pako; uzitunze katika moyo wako.
22 Porque son vida a los que las hallan; y medicina a toda su carne.
Maana maneno yangu ni uzima kwa wenye kuyapata na afya katika mwili wao.
23 Sobre toda cosa guardada, guarda tu corazón; porque de él mana la vida.
Ulinde salama moyo wako na uukinge kwa bidii zote; kwa kuwa katika moyo hububujika chemichemi za uzima.
24 Aparta de ti la perversidad de la boca; y la iniquidad de labios aleja de ti.
Jiepushe na kauli za udanganyifu na ujiepushe na mazungumzo ya ufisadi.
25 Tus ojos miren lo recto; y tus párpados enderecen tu camino delante de ti.
Macho yako yatazame mbele kwa unyoofu na kwa uthabiti tazama mbele sawasawa.
26 Pesa la vereda de tus pies; y todos tus caminos sean ordenados.
Usawazishe pito la mguu wako; na njia zako zote zitakuwa salama.
27 No te apartes a diestra, ni a siniestra: aparta tu pie del mal.
Usigeuke upande wa kulia au kushoto; ondoa mguu wako mbali na uovu.