< Proverbios 26 >

1 Como la nieve en el verano, y la lluvia en la segada, así conviene al insensato la honra.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 Como el gorrión andar vagabundo, y como la golondrina volar, así la maldición sin causa nunca vendrá.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 El azote para el caballo, y el cabestro para el asno, y la vara para el cuerpo del insensato.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Nunca respondas al insensato conforme a su fatuidad, porque no seas como él también tú.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Responde al insensato conforme a su fatuidad, porque no se estime sabio en su opinión.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 El que corta los pies, beberá el daño; y el que envía algo por la mano del insensato.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Alzád las piernas del cojo: así es el proverbio en la boca del insensato.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Como quien liga la piedra en la honda, así es el que da honra al insensato.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Espinas hincadas en mano de embriagado: tal es el proverbio en la boca de los insensatos.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 El Grande cria todas las cosas; y al insensato da la paga, y a los transgresores da el salario.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 Como perro que vuelve a su vómito: así el insensato que segunda su fatuidad.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 ¿Has visto hombre sabio en su opinión? más esperanza hay del insensato que de él.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 Dice el perezoso: El león está en el camino: el león está en las calles.
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 Las puertas se revuelven en su quicio, y el perezoso en su cama.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 Esconde el perezoso su mano en el seno: cánsase de tornarla a su boca.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 Más sabio es el perezoso en su opinión, que siete que le den consejo.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 El que pasando se enoja en el pleito ajeno, es como el que toma al perro por las orejas.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Como el que enloquece, y echa llamas, y saetas, y muerte,
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 Tal es el hombre que daña a su amigo, y dice: Cierto, burlaba.
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Sin leña, el fuego se apagará; y donde no hubiere chismoso, cesará la contienda.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 El carbón para brasas; y la leña para el fuego; y el hombre rencilloso para encender contienda.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 Las palabras del chismoso parecen blandas: mas ellas entran hasta lo secreto del vientre.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Plata de escorias echada sobre tiesto son los labios encendidos, y el corazón malo.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 Otro parece en los labios el que aborrece: mas en su interior pone engaño:
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 Cuando hablare amigablemente, no le creas; porque siete abominaciones están en su corazón.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Encúbrese el odio en el desierto: mas su malicia será descubierta en la congregación.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 El que cavare sima, en ella caerá; y el que revuelve la piedra, a él volverá.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 La falsa lengua al que atormenta aborrece; y la boca lisonjera hace resbaladero.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Proverbios 26 >