< Proverbios 24 >
1 No tengas envidia de los hombres malos: ni desees estar con ellos.
Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
2 Porque su corazón piensa en robar; e iniquidad hablan sus labios.
kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3 Con sabiduría se edificará la casa; y con prudencia se afirmará.
Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4 Y con ciencia las cámaras se henchirán de todas riquezas preciosas y hermosas.
Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5 El hombre sabio es fuerte; y el hombre entendido es valiente de fuerza.
Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6 Porque con industrias harás la guerra; y la salud está en la multitud de los consejeros.
maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7 Alta está para el insensato la sabiduría: en la puerta no abrirá su boca.
Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8 Al que piensa mal hacer, al tal, hombre de malos pensamientos le llamarán.
Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9 El mal pensamiento del insensato es pecado; y abominación a los hombres el burlador.
Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10 Si fueres flojo en el día de trabajo, tu fuerza será angosta.
Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
11 ¿Detenerte has de escapar los que son tomados para la muerte, y los que son llevados al degolladero?
Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
12 Si dijeres: Ciertamente no lo supimos: ¿el que pesa los corazones no lo entenderá? El que mira por tu alma él lo conocerá, el cual dará al hombre según sus obras.
Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
13 Come, hijo mío, de la miel, porque es buena; y del panal dulce a tu paladar:
Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
14 Tal será el conocimiento de la sabiduría a tu alma, si la hallares; y al fin tu esperanza no será cortada.
Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
15 O! impío, no aseches a la tienda del justo: no saquees su acostadero:
Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
16 Porque siete veces cae el justo, y se torna a levantar: mas los impíos caerán en el mal.
Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17 Cuando cayere tu enemigo, no te huelgues; y cuando tropezare, no se alegre tu corazón:
Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18 Porque Jehová no lo mire, y le desagrade; y aparte de sobre él su enojo.
au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19 No te entremetas con los malignos, ni tengas envidia de los impíos:
Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20 Porque para el malo no habrá buen fin; y la candela de los impíos será apagada.
maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21 Teme a Jehová, hijo mío, y al rey: no te entremetas con los inmutadores:
Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22 Porque su quebrantamiento se levantará de repente: ¿y el quebrantamiento de ambos quién lo comprenderá?
maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23 También estas cosas pertenecen a los sabios. Tener respeto a personas en el juicio, no es bueno.
Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24 El que dijere al malo, justo eres: los pueblos le maldecirán, y las naciones le detestarán:
Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25 Mas los que le reprenden, serán agradables; y sobre ellos vendrá bendición de bien.
Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26 Los labios serán besados, del que responde palabras rectas.
Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27 Apareja de fuera tu obra, y dispónela en tu heredad; y después edificarás tu casa.
Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28 No seas testigo sin causa contra tu prójimo; y no lisonjees con tus labios.
Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
29 No digas: Como me hizo, así le haré: daré el pago al varón según su obra.
Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
30 Pasé junto a la heredad del hombre perezoso, y junto a la viña del hombre falto de entendimiento.
Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
31 Y he aquí que por toda ella habían ya crecido espinas, ortigas habían ya cubierto su superficie, y su cerca de piedra estaba ya destruida.
Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Y yo miré, y púse lo en mi corazón: lo ví, y recibí enseñanza.
Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
33 Tomando un poco de sueño, cabeceando otro poco, poniendo mano sobre mano otro poco para volver a dormir:
Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
34 Vendrá como caminante, tu necesidad; y tu pobreza como hombre de escudo.
na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.