< Job 7 >

1 Ciertamente tiempo determinado tiene el hombre sobre la tierra; y sus días son como los días del jornalero.
Je mtu hana kazi ngumu juu ya nchi? Je siku zake si kama siku za mwajiriwa?
2 Como el siervo desea la sombra, y como el jornalero espera su trabajo:
Kama mtumwa atamaniye sana kivuli cha jioni, kama mwajiriwa atafutaye ujira wake -
3 Así poseo yo los meses de vanidad, y las noches del trabajo me dieron por cuenta.
hivyo nami nimeumbwa kuvumilia miezi ya taabu; Nami nimepewa taabu - zimeujaza usiku.
4 Cuando estoy acostado, digo: ¿Cuándo me levantaré? Y mide mi corazón la noche, y estoy harto de devaneos hasta el alba.
Hapo nilalapo chini, najiuliza mwenyewe, 'Lini nitatoka kitandani na lini usiku utatoweka?' Nimejawa na kujitupa huku na huko hadi mwanzo wa siku.
5 Mi carne está vestida de gusanos, y de terrones de polvo: mi piel rompida y abominable.
Mwili wangu umevikwa minyoo na madonda yenye vumbi; maumivu katika ngozi yangu yamekuwa magumu na kisha hutoweka na huendelea tena.
6 Mis días fueron más ligeros, que la lanzadera del tejedor; y fenecieron sin esperanza.
Siku zangu zinakimbia kuliko chombo cha kufumia; zinapita bila tumaini.
7 Acuérdate que mi vida es un viento; y que mis ojos no volverán para ver el bien.
Mungu, anakumbuka kwamba maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona mema tena.
8 Los ojos de los que [ahora] me ven, nunca más me verán: tus ojos serán sobre mí, y dejaré de ser.
Jicho lake Mungu, huyo anionaye mimi, halitaniangalia tena; Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako.
9 La nube se acaba, y se va: así es el que desciende al sepulcro, que nunca más subirá. (Sheol h7585)
kama vile wingu liishavyo na kutoweka, hivyo wale waendao sheoli hawatarudi tena kabisa. (Sheol h7585)
10 No tornará más a su casa, ni su lugar le conocerá más.
Yeye hatarudi tena nyumbani kwake, wala mahali pake hapatamtambua tena.
11 Por tanto yo no detendré mi boca, mas hablaré con la angustia de mi espíritu, y quejarme he con la amargura de mi alma.
Kwa sababu hiyo sitakizuia kinywa changu; Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu.
12 ¿Soy yo la mar, o alguna ballena que me pongas guardia?
Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?
13 Cuando digo: Mi cama me consolará, mi cama me quitará mis quejas:
Hapo nisemapo, 'kitanda changu kitanifariji, na malazi yangu yatatuliza manung'uniko yangu,'
14 Entonces me quebrantarás con sueños, y me turbarás con visiones.
halafu unitishapo kwa ndoto na kunitisha kwa maono,
15 Y mi alma tuvo por mejor el ahogamiento; y la muerte más que a mis huesos.
ili nichague kunyongwa na kufa kuliko kulinda mifupa yangu hii.
16 Abominé la vida, no quiero vivir para siempre: déjame, pues que mis días son vanidad.
Ninayachukia kabisa maisha yangu; sitamani siku zote kuwa hai; usinisumbue maana siku zangu hazifai.
17 ¿Qué es el hombre para que le engrandezcas, y que pongas sobre él tu corazón;
Je mtu ni nini hata ukatia bidii kwake, na ukaweka akili yako kwake,
18 Y que le visites todas las mañanas, y todos los momentos le pruebes?
na kumwangalia kila asubuhi, na kumjaribu kila mara?
19 ¿Hasta cuándo no me dejarás, ni me soltarás hasta que trague mi saliva?
Je itachukuwa muda gani kabla hujaacha kuniangalia, wala kunisumbua muda wa kutosha kwaajili ya kumeza mate yangu?
20 Pequé: ¿qué te haré, oh guardador de los hombres? ¿Por qué me has puesto contrario a ti, y qué a mí mismo sea pesadumbre?
Hata kama nimefanya dhambi, itakusaidia nini, wewe ulindaye wanadamu? Kwa nini umenifanya shabaha yako, kiasi kwamba nimekuwa mzigo kwako?
21 ¿Y por qué no quitas mi rebelión, y perdonas mi iniquidad? porque ahora dormiré en el polvo; y buscarme has de mañana, y no seré hallado.
Kwa nini hunisamehi makosa yangu na kuniondolea uovu wangu? kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; na wewe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwako.”

< Job 7 >