< Job 40 >

1 Y respondió Jehová a Job, y dijo:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 ¿Es sabiduría contender con el Omnipotente? El que disputa con Dios, responda a esto.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Y respondió Job a Jehová, y dijo:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 He aquí, que yo soy vil, ¿qué te responderé? Mi mano pongo sobre mi boca.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Una vez hablé, y no responderé; y dos veces; mas no tornaré a hablar.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Y respondió Jehová a Job desde la oscuridad, y dijo:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Cíñete ahora, como varón, tus lomos: yo te preguntaré, y házme saber.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 ¿Invalidarás tú también mi juicio? ¿condenarme has a mi para justificarte a ti?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 ¿Tienes tú brazo como Dios? ¿y tronarás tú con voz como él?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Ahora atavíate de magestad y de alteza, y vístete de honra y de hermosura.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Esparce furores de tu ira, y mira a todo soberbio, y abátele.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Mira a todo soberbio, y póstrale; y quebranta los impíos en su asiento.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Encúbrelos a todos en el polvo; y ata sus rostros en oscuridad;
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Y yo también te confesaré, que tu diestra te salvará.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 He aquí ahora Behemot, al cual yo hice contigo; yerba come como buey.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 He aquí ahora que su fuerza está en sus lomos; y su fortaleza en el ombligo de su vientre:
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 Su cola mueve como un cedro; y los nervios de sus genitales son entretejidos:
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 Sus huesos son fuertes como acero, y sus miembros como barras de hierro:
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Él es la cabeza de los caminos de Dios: el que le hizo le acercará de su espada.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Ciertamente los montes llevan renuevo para él; y toda bestia del campo retoza allá.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Debajo de las sombras se echará, en lo oculto de las cañas, y de los lugares húmedos.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Los árboles sombríos le cubren con su sombra; los sauces del arroyo le cercan.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 He aquí que él robará el río que no corra; y confíase que el Jordán pasará por su boca.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 El le tomará por sus ojos en los tropezaderos, y le horadará la nariz.
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >