< Job 40 >
1 Y respondió Jehová a Job, y dijo:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 ¿Es sabiduría contender con el Omnipotente? El que disputa con Dios, responda a esto.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Y respondió Job a Jehová, y dijo:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 He aquí, que yo soy vil, ¿qué te responderé? Mi mano pongo sobre mi boca.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Una vez hablé, y no responderé; y dos veces; mas no tornaré a hablar.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Y respondió Jehová a Job desde la oscuridad, y dijo:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Cíñete ahora, como varón, tus lomos: yo te preguntaré, y házme saber.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 ¿Invalidarás tú también mi juicio? ¿condenarme has a mi para justificarte a ti?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 ¿Tienes tú brazo como Dios? ¿y tronarás tú con voz como él?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Ahora atavíate de magestad y de alteza, y vístete de honra y de hermosura.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Esparce furores de tu ira, y mira a todo soberbio, y abátele.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Mira a todo soberbio, y póstrale; y quebranta los impíos en su asiento.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Encúbrelos a todos en el polvo; y ata sus rostros en oscuridad;
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Y yo también te confesaré, que tu diestra te salvará.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 He aquí ahora Behemot, al cual yo hice contigo; yerba come como buey.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 He aquí ahora que su fuerza está en sus lomos; y su fortaleza en el ombligo de su vientre:
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Su cola mueve como un cedro; y los nervios de sus genitales son entretejidos:
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Sus huesos son fuertes como acero, y sus miembros como barras de hierro:
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Él es la cabeza de los caminos de Dios: el que le hizo le acercará de su espada.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Ciertamente los montes llevan renuevo para él; y toda bestia del campo retoza allá.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Debajo de las sombras se echará, en lo oculto de las cañas, y de los lugares húmedos.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 Los árboles sombríos le cubren con su sombra; los sauces del arroyo le cercan.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 He aquí que él robará el río que no corra; y confíase que el Jordán pasará por su boca.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 El le tomará por sus ojos en los tropezaderos, y le horadará la nariz.
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?