< Salmos 92 >
1 Bueno es alabar a Yavé Y cantar salmos a tu Nombre, oh ʼElyón.
Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato. Ni vyema kumshukuru Bwana na kuliimbia jina lako, Ee Uliye Juu Sana,
2 Anunciar por la mañana tu misericordia Y tu fidelidad cada noche
kuutangaza upendo wako asubuhi, na uaminifu wako wakati wa usiku,
3 Con el decacordio y el salterio, Con el armonioso tono del arpa.
kwa zeze yenye nyuzi kumi na kwa sauti ya kinubi.
4 Porque Tú, oh Yavé, me alegraste con lo que hiciste. Por las obras de tus manos doy gritos de júbilo.
Ee Bwana, kwa kuwa matendo yako yamenifurahisha, nitaziimba kwa shangwe kazi za mikono yako.
5 ¡Cuán grandes son tus obras, oh Yavé! Tus pensamientos son muy profundos.
Ee Bwana, tazama jinsi yalivyo makuu matendo yako, tazama jinsi yalivyo ya kina mawazo yako!
6 El hombre necio no sabe Y el insensato no entiende esto:
Mjinga hafahamu, mpumbavu haelewi,
7 Que cuando los perversos brotan como hierba, Y florecen todos los que hacen iniquidad, [Solo sucede] para que sean destruidos eternamente.
ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.
8 Pero Tú, oh Yavé, eres altísimo para siempre.
Bali wewe, Ee Bwana, utatukuzwa milele.
9 Porque ya veo que tus enemigos, oh Yavé, Ya veo que tus enemigos perecen. Son dispersados todos los obradores de iniquidad.
Ee Bwana, hakika adui zako, hakika adui zako wataangamia. Wote watendao mabaya watatawanyika.
10 Pero Tú aumentarás mi fuerza como la del búfalo. Seré ungido con aceite fresco.
Umeitukuza pembe yangu kama ile ya nyati dume, mafuta mazuri yamemiminwa juu yangu.
11 Y mis ojos mirarán por encima de mis enemigos. Mis oídos escucharán Con respecto a los perversos que se levantan contra mí.
Macho yangu yamewaona adui zangu wakishindwa, masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu.
12 El justo florecerá como la palmera. Crecerá como un cedro en el Líbano.
Wenye haki watastawi kama mtende, watakuwa kama mwerezi wa Lebanoni,
13 Plantados en la Casa de Yavé, Florecerán en los patios de nuestro ʼElohim.
waliopandwa katika nyumba ya Bwana, watastawi katika nyua za Mungu wetu.
14 Aun en la vejez darán fruto. Estarán llenos de savia y muy verdes
Wakati wa uzee watakuwa bado wanazaa matunda, watakuwa wabichi tena wamejaa nguvu,
15 Para manifestar que Yavé es recto. Mi Roca es. En Él no hay injusticia.
wakitangaza, “Bwana ni mkamilifu; yeye ni Mwamba wangu, na ndani yake hamna uovu.”