< Salmos 80 >

1 Oh Pastor de Israel, escucha. Tú, que pastoreas a José como un rebaño, Tú, que estás entronizado entre querubines, ¡Resplandece!
Usikie, Mchungaji wa Israel, wewe uliye muongoza Yusufu kama kundi; wewe uketiye juu ya makerubi, utuangazie!
2 Delante de Efraín, de Benjamín y de Manasés, Despierta tu poder Y ven a salvarnos.
Machoni pa Efraimu na Benjamini na Manase, uziinue nguvu zako; njoo na utuokoe.
3 Restáuranos, oh ʼElohim. Haz resplandecer tu rostro, Y seremos salvos.
Mungu, uturejeshe sisi; uangaze uso wako juu yetu, nasi tutaokolewa.
4 Oh Yavé, ʼElohim de las huestes, ¿Hasta cuándo estarás airado contra la oración de tu pueblo?
Yahwe Mungu wa majeshi, mpaka lini utawakasirikia watu wako wanapoomba?
5 Los alimentaste con pan de lágrimas. Les diste a beber lágrimas en abundancia.
Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
6 Nos conviertes en escarnio de nuestros vecinos, Y nuestros enemigos se burlan de nosotros.
Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.
7 Oh ʼElohim de las huestes, restáuranos. Haz resplandecer tu rostro, Y seremos salvos.
Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; nasi tutaokolewa.
8 Trajiste una vid de Egipto. Expulsaste las naciones Y la plantaste.
Wewe ulileta mzabibu kutoka Misri; ukawafukuza mataifa na ukaupanda.
9 Limpiaste delante de ella. Desarrolló profunda raíz y llenó la tierra.
Uliisafisha ardhi kwa ajil yake; nao ulipata mzizi na kuijaza nchi.
10 Las montañas fueron cubiertas con su sombra, Y con sus ramas los cedros de ʼElohim.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
11 Extendió sus ramas hasta el mar Y hasta el río sus retoños.
Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
12 ¿Por qué derribaste sus cercas De modo que recogen sus frutos todos los que pasan por el camino?
Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
13 El jabalí la destroza, Y las bestias del campo la devoran.
Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
14 Oh ʼElohim de las huestes, vuelve, te rogamos. Mira desde el cielo, considera, Y cuida esta viña.
Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
15 La cepa que plantó tu mano derecha Y la rama que fortaleciste para Ti
Huu ni mzizi ambao mkono wako wa kuume umeupanda, mashina ambayo wewe uliyafanya yakue.
16 Está quemada con fuego y cortada. Perezcan por la reprensión de tu rostro.
Yamekatwa na kuchomwa; yameangamia kwa sababu ya kukemea kwako.
17 Que tu mano sea sobre el varón de tu mano derecha, Sobre el Hijo de Hombre que para Ti fortaleciste.
Mkono wako na uwe juu ya mtu aliye mkono wako wa kuume, kwa mwana wa mtu uliyemfanya imara kwa ajili yako mwenyewe.
18 Así no nos apartaremos de Ti. Revívemos e invocaremos tu Nombre.
Ndipo hatuta kuacha wewe; utuhuishe, nasi tutaliita jina lako.
19 Oh Yavé, ʼElohim de las huestes, restáuranos. Que tu rostro resplandezca, Y seremos salvos.
Yahwe, Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; utuangazie nuru ya uso wako, nasi tutaokolewa.

< Salmos 80 >