< Salmos 55 >
1 Oh ʼElohim, escucha mi oración, Y no te escondas de mi súplica.
Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, sikiliza maombi yangu, wala usidharau hoja yangu.
2 Está atento y respóndeme. Estoy inquieto y conturbado en mi oración
Nisikie na unijibu. Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa
3 A causa de la voz del enemigo. Por la opresión del perverso, Porque bajan aflicción sobre mí, Y me persiguen con furor.
kwa sauti ya adui, kwa kukaziwa macho na waovu, kwa sababu wananiletea mateso juu yangu na kunitukana kwa hasira zao.
4 Mi corazón se retuerce dentro de mí. Me asaltan terrores de [la] muerte.
Moyo wangu umejaa uchungu, hofu ya kifo imenishambulia.
5 Temor y temblor vienen sobre mí. El terror me cubre,
Woga na kutetemeka vimenizunguka, hofu kuu imenigharikisha.
6 Y digo: ¡Oh, si yo tuviera alas como una paloma! Volaría yo y descansaría.
Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa! Ningeruka niende mbali kupumzika.
7 Ciertamente huiría lejos. Viviría en el desierto. (Selah)
Ningalitorokea mbali sana na kukaa jangwani,
8 Me apresuraría a escapar del viento borrascoso de la tempestad, Del aguacero fuerte y la tormenta.
ningaliharakisha kwenda mahali pa salama, mbali na tufani kali na dhoruba.”
9 Destrúyelos, oh ʼAdonay, confunde sus lenguas, Porque vi en la ciudad violencia y disputa.
Ee Bwana, uwatahayarishe waovu na uwachanganyishie semi zao, maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.
10 Día y noche rondan sobre sus muros. La iniquidad y la aventura están en medio de ella.
Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake, uovu na dhuluma vimo ndani yake.
11 Destrucción hay dentro de ella. Opresión y engaño no se apartan de sus calles.
Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini, vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.
12 Porque no es un enemigo el que me agravia. Si fuera así, lo soportaría. Ni se levantó contra mí el que me aborrece. Podría ocultarme de él.
Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione.
13 Sino tú, un hombre igual a mí, Mi compañero, mi íntimo amigo.
Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu,
14 Juntos teníamos dulce comunión, Y con intimidad andábamos en la Casa de ʼElohim.
ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri, tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.
15 Que la muerte los sorprenda, Que desciendan vivos al Seol, Porque hay maldad en su habitación, en medio de ellos. (Sheol )
Kifo na kiwajie adui zangu ghafula, na washuke kuzimu wangali hai, kwa maana uovu upo ndani yao. (Sheol )
16 Pero yo clamaré a ʼElohim, Y Yavé me salvará.
Lakini ninamwita Mungu, naye Bwana huniokoa.
17 Al llegar la noche, por la mañana y a mediodía Me quejaré y gemiré, Y Él escuchará mi voz.
Jioni, asubuhi na adhuhuri ninalia kwa huzuni, naye husikia sauti yangu.
18 Él rescata en paz mi alma del ataque contra mí, Aunque muchos se enfrenten contra mí.
Huniokoa nikawa salama katika vita vilivyopangwa dhidi yangu, ingawa watu wengi hunipinga.
19 ʼEL escuchará y los afligirá, Él, Quien está entronizado desde tiempo antiguo. (Selah) Porque ellos no cambian, Por tanto no temen a ʼElohim.
Mungu anayemiliki milele, atawasikia na kuwaadhibu, watu ambao hawabadilishi njia zao, wala hawana hofu ya Mungu.
20 [El inicuo] extiende sus manos Contra los que estaban en paz con él. Viola su pacto.
Mwenzangu hushambulia rafiki zake, naye huvunja agano lake.
21 Su boca fue más blanda que mantequilla, Pero hay contienda en su corazón. Más suaves que aceite son sus palabras, Pero son como espadas desenvainadas.
Mazungumzo yake ni laini kama siagi, hata hivyo vita vimo moyoni mwake. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.
22 Echa sobre Yavé tu carga, Y Él te sustentará. Jamás dejará caído al justo.
Mtwike Bwana fadhaa zako, naye atakutegemeza, hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.
23 Oh ʼElohim, Tú los harás bajar a la fosa de destrucción. Los sanguinarios y engañadores no vivirán la mitad de sus días. Pero yo confío en Ti.
Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha waovu katika shimo la uharibifu. Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila, hawataishi nusu ya siku zao. Lakini mimi ninakutumaini wewe.