< Salmos 44 >
1 Oh ʼElohim, escuchamos con nuestros oídos, Nos contaron nuestros antepasados Las obras que Tú hiciste en sus días, En los tiempos antiguos.
Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
2 Con tu mano expulsaste a las naciones Para establecerlos a ellos. Abatiste a los pueblos y los echaste.
Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3 No poseyeron la tierra por su espada, Ni los libró su brazo, Sino tu mano derecha, tu brazo y la luz de tu rostro, Porque te complaciste en ellos.
Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4 Tú eres mi Rey, oh ʼElohim. ¡Ordena las victorias de Jacob!
Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5 Por medio de Ti sacudiremos a nuestros enemigos. En tu Nombre pisotearemos a los que se levantan contra nosotros.
Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6 Porque no confiaré en mi arco, Ni mi espada me salvará.
Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7 Pero Tú nos salvaste de nuestros adversarios Y avergonzaste a los que nos aborrecen.
Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8 En ʼElohim nos gloriaremos todo el día Y alabaremos tu Nombre para siempre. (Selah)
Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
9 Pero nos desechaste y nos avergonzaste. No sales con nuestros ejércitos.
Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10 Nos haces retroceder del adversario. Los que nos aborrecen nos saquean.
Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11 Nos entregas como ovejas para el matadero Y nos esparciste entre las naciones.
Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 Vendes a tu pueblo por nada. Ningún beneficio exiges por ellos.
Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 Nos convertiste en oprobio de nuestros vecinos, En escarnio y burla de los que nos rodean.
Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 Nos pusiste como refrán entre las naciones, Un objeto de burla en medio de los pueblos.
Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
15 Todo el día mi deshonor está delante de mí Y la confusión cubre mi cara,
Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 Por la voz del que me critica y deshonra Por causa del enemigo y del vengativo.
kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 Todo esto nos vino, Pero no nos olvidamos de Ti, Ni fuimos infieles a tu Pacto.
Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 Nuestro corazón no se volvió atrás, Ni nuestros pasos se desviaron de tu senda.
Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 Pero Tú nos aplastaste en un sitio de chacales, Y nos cubriste con la sombra de muerte.
Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 Si nos olvidamos del Nombre de nuestro ʼElohim O alzamos nuestras manos a un ʼelohim extraño,
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 ¿ʼElohim no demandaría esto? Porque Él conoce los secretos del corazón.
Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 Pero por tu causa nos matan cada día. Somos considerados como ovejas para el matadero.
Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 Despiértate, ʼAdonay. ¿Por qué duermes? Despiértate, no nos rechaces para siempre.
Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24 ¿Por qué escondes tu rostro Y te olvidas de la aflicción y de nuestra opresión?
Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 Porque nuestra alma está agobiada hasta el polvo Y nuestro cuerpo está pegado a la tierra.
Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26 Levántate, sé nuestra Ayuda. Redímenos por tu misericordia.
Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.