< Salmos 34 >
1 Bendeciré a Yavé en todo tiempo. Su alabanza estará de continuo en mi boca.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 En Yavé se gloriará mi alma. Lo oirán los mansos y se alegrarán.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Engrandezcan a Yavé conmigo, Y exaltemos juntos su Nombre.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 Busqué a Yavé y Él me respondió, Y me libró de todos mis temores.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Los que miraron a Él fueron iluminados, Y sus semblantes nunca serán avergonzados.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Este pobre clamó, Y Yavé lo escuchó, Y lo salvó de todas sus angustias.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 El Ángel de Yavé acampa alrededor de los que le temen, Y los rescata.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Prueben y vean que Yavé es bueno. ¡Cuán feliz es el varón que confía en Él!
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Teman a Yavé, ustedes sus santos, Porque nada falta a los que le temen.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Los cachorros de león necesitan y sufren hambre, Pero los que buscan a Yavé no carecen de ningún bien.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Vengan, hijos, escúchenme. Les enseñaré el temor a Yavé.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 ¿Quién es el hombre que desea vida, Que desea muchos días para ver el bien?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Guarda tu boca del mal Y tus labios de hablar engaño.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Apártate del mal y haz el bien. Busca la paz y persíguela.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 Los ojos de Yavé están hacia los justos, Y sus oídos atentos al clamor de ellos.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 El rostro de Yavé está contra los perversos, Para cortar su memoria de la tierra.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Claman los justos, Y Yavé los oye Y los libra de todas sus angustias.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Cercano está Yavé a los quebrantados de corazón, Y salva a los contritos de espíritu.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Muchas son las aflicciones del justo, Pero de todas ellas lo libra Yavé.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Él guarda todos sus huesos. Ni uno de ellos es quebrado.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 Matará al malo la maldad, Y los que aborrecen al justo serán culpables.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 Yavé redime la vida de sus esclavos. No serán condenados cuantos en Él confían.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.