< Salmos 21 >
1 Oh Yavé, el rey se alegrará en tu poder, Y en tu salvación ¡cuánto se regocijará!
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. Mfalme anashangilia katika uweza wako, Yahwe! Ni kwa namna kuu anashangilia katika wokovu uliouleta!
2 Le diste el deseo de su corazón Y no le retuviste la petición de sus labios. (Selah)
Wewe umempa yeye matamanio ya moyo wake na hauja mkatalia maombi midomo yake.
3 Con bendiciones de bien saliste a su encuentro. Corona de oro puro pusiste en su cabeza.
Kwa kuwa wewe unamletea baraka nyingi; wewe uliweka katika kichwa chake taji ya dhahabu iliyo safi kabisa.
4 Vida te pidió, Y se la concediste, Largura de días, eternamente y para siempre.
Yeye alikuomba wewe maisha; ukampatia maisha; wewe ulimpatia maisha malefu milele na milele.
5 Grande es su gloria por tu salvación. Pusiste sobre él honor y majestad.
Yeye utukufu wake ni mkuu kwa sababu ya ushindi wako; wewe umemuwekea mapambo na enzi.
6 Lo bendijiste para siempre. Lo llenaste de alegría con tu Presencia
Kwa kuwa unampatia yeye baraka za kudumu; unamfurahisha kwa furaha ya uwepo wako.
7 Por cuanto el rey confía en Yavé. Por la misericordia de ʼElyón, no será conmovido.
Kwa kuwa Mfalme humwamini Yahwe; kwa kupitia uaminifu wa agano la aliye juu zaidi yeye hataondolewa.
8 Tu mano alcanzará a todos tus enemigos. Tu mano derecha alcanzará a los que te aborrecen.
Mkono wako utawakamata adui zangu wote wote; mkono wako wa kuume utawakamata wale wote wanao kuchukia.
9 Los pondrás en horno de fuego en el tiempo de tu ira. Yavé los deshará en su ira, Y el fuego los consumirá.
Wakati wa hasira yako, wewe utawachoma kama katika tanuru la moto. Yahwe atawamaliza wao katika hasira yake, na moto utawateketeza upesi wao.
10 Destruirás su producto de la tierra, Y su descendencia de entre los hijos de hombres.
Wewe utawaangamiza watoto wao duniani na ukoo wao kutoka katika mrorongo wa wanadamu.
11 Porque tramaron el mal contra Ti. Fraguaron un complot, Pero no prevalecerán.
Kwa kuwa walikusudia kukufanyia mambo maovu wewe; wao walitunga njama ambayo kwayo hawawezi kufanikiwa!
12 Pues Tú les harás volver la espalda Al apuntar tu arco contra sus rostros.
Kwa kuwa wewe utawarudisha nyuma; wewe utafyatua upinde wako mbele yao.
13 ¡Engrandécete, oh Yavé, con tu fortaleza! Cantaremos y alabaremos tu poderío.
Uninuliwe, Yahwe, katika uweza wako; tutaimba na kusifu nguvu zako.