< Salmos 140 >
1 Rescátame, oh Yavé, de hombres perversos. Guárdame de hombres violentos
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
2 Que maquinan cosas malas en [sus] corazones. Continuamente promueven guerras,
ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
3 Afilan su lengua como serpiente. Veneno de víbora hay debajo de sus labios. (Selah)
Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
4 Guárdame, oh Yavé, de las manos de los perversos. Guárdame de hombres violentos, Que se proponen que vacilen mis pies.
Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
5 Soberbios esconden trampa y cuerdas contra mí, Junto al sendero me extienden una red. (Selah)
Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
6 Digo a Yavé: Tú eres mi ʼElohim. Presta oído, oh Yavé, a la voz de mis súplicas.
Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
7 Oh Yavé ʼAdonay, Fortaleza de mi salvación, Cubriste mi cabeza en el día de la batalla.
Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
8 No concedas, oh Yavé, los deseos del perverso. No promuevas su designio de ser ellos exaltados. (Selah)
Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
9 En cuanto a la cabeza de los que me rodean, Cúbralos la perversidad de sus propios labios.
Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
10 Que caigan sobre ellos carbones encendidos. Que sean echados al fuego En abismos profundos de donde no puedan salir.
Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
11 Que el difamador no sea establecido en la tierra. Que el mal cace velozmente al varón violento.
Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
12 Yo sé que Yavé defiende la causa del afligido, Y la justicia para el pobre.
Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
13 Ciertamente los justos darán gracias a tu Nombre, Los rectos vivirán en tu Presencia.
Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.