< Salmos 135 >
1 Alaben el Nombre de Yavé. Alábenlo, esclavos de Yavé,
Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
2 Ustedes quienes están en la Casa de Yavé, En los patios de la Casa de nuestro ʼElohim.
ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 ¡Aleluya, porque Yavé es bueno! Canten salmos a su Nombre, Porque [eso] es agradable.
Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
4 Porque YA escogió a Jacob para Él, A Israel como su posesión.
Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
5 Porque yo sé que Yavé es grande, Y que nuestro ʼAdonay está por encima de todos los ʼelohim.
Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
6 Yavé hace todo lo que quiere, Tanto en el cielo como en la tierra, En los mares y en todos los abismos.
Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
7 Él impulsa Para que las nieblas suban desde los confines de la tierra. Produce relámpagos para la lluvia, Saca de sus tesoros el viento.
Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
8 Él fue el que mató a los primogénitos de Egipto, Tanto del hombre como del animal.
Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9 En medio de Ti, oh Egipto, envió señales y prodigios, Contra Faraón y todos sus esclavos.
Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Destruyó a muchas naciones, Y mató a reyes poderosos:
Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11 A Sehón rey de los amorreos, A Og rey de Basán, Y a todos los reyes de Canaán.
Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
12 Dio la tierra de ellos Como heredad a su pueblo Israel.
Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
13 Oh Yavé, eterno es tu Nombre. Tu memoria, oh Yavé, por todas las generaciones.
Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
14 Porque Yavé juzgará a su pueblo Y tendrá compasión de sus esclavos.
Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
15 Los ídolos de las naciones son [de] plata y oro, Obra de manos de hombre.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
16 Tienen bocas, pero no hablan. Tienen ojos, pero no ven.
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
17 Tienen orejas, pero no oyen, Tampoco hay aliento en sus bocas.
zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
18 Los que las hacen son semejantes a ellos, Y todo el que confía en ellos.
Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
19 ¡Oh casa de Israel, bendiga a Yavé! ¡Oh casa de Aarón, bendiga a Yavé!
Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
20 ¡Oh casa de Leví, bendiga a Yavé! ¡Los que temen a Yavé, bendigan a Yavé!
Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
21 ¡Desde Sion, bendito sea Yavé, Quien mora en Jerusalén! ¡Aleluya!
Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.