< Salmos 120 >
1 En mi angustia clamé a Yavé, Y Él me respondió.
Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe, naye akanijibu.
2 Oh Yavé, libra mi vida de labios mentirosos, De una lengua engañadora.
Uiokoe nasfi yangu, yahwe, dhidi ya wale wadanganyao kwa midomo yao na wanenao hila kwa ndimi zao.
3 ¿Qué se te dará, O qué más se te hará, Oh lengua engañosa?
Yahwe atawaadhibu vipi, na atawafanyia kitu gani zaidi, ninyi mlio na ulimi mdanganyifu?
4 Agudas flechas de guerrero, [Forjadas] con brasas de enebro.
Atawaadhibu kwa mishale ya shujaa iliyo nolewa kwa makaa ya moto ya mretemu.
5 ¡Ay de mí, porque vivo desterrado en Mesec, Y habito entre las tiendas de Cedar!
Ole wangu mimi kwa sababu ninaishi kwa muda Mesheki; huko nyuma niliishi kati ya maskani ya Kedari.
6 Mucho tiempo estuvo mi alma Con los que aborrecen la paz.
Kwa muda mrefu sana niliisha na wale waichukiao amani.
7 Yo soy pacífico, pero cuando hablo, Ellos me declaran la guerra.
Nipo kwa ajili ya amani, lakini ninenapo, wao wako kwa ajili ya vita.