< Salmos 107 >

1 ¡Den gracias a Yavé, Porque Él es bueno, Porque para siempre es su misericordia!
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Que lo digan los redimidos de Yavé, Los que redimió del poder del adversario,
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
3 Y los que congregó de las tierras, Del oriente y del occidente, del norte y del sur.
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Ellos vagaron en un desierto, en región despoblada. No hallaron un camino hacia una ciudad habitada.
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
5 Tenían hambre y sed. Sus almas desfallecían en ellos.
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
6 Pero clamaron a Yavé en su angustia. Él los libró de sus aflicciones.
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
7 Los condujo por un camino recto Para ir a una ciudad habitada.
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
8 ¡Den gracias a Yavé por su misericordia Y por sus maravillas para los hijos de [los ]hombres!
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
9 Porque Él sacia al alma que tiene sed Y llena de bien al alma que tiene hambre.
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
10 Vivían en oscuridad y sombra de muerte, Prisioneros en aflicción y cadenas,
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
11 Por cuanto fueron rebeldes a las Palabras de ʼEL Y trataron con desprecio el consejo del ʼElyón.
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
12 Por tanto Él quebrantó sus corazones con trabajo. Cayeron y no hubo quien los ayudara.
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
13 Pero en su angustia clamaron a Yavé, Él los libró de sus aflicciones.
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
14 Los sacó de la oscuridad y de la sombra de muerte, Y rompió sus ataduras.
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
15 ¡Den gracias a Yavé por su misericordia, Y por sus maravillas para los hijos de [los] hombres!
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
16 Porque quebró las puertas de bronce, Y desmenuzó los cerrojos de hierro.
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Fueron afligidos los necios a causa de su camino rebelde, Y a causa de sus iniquidades fueron afligidos.
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
18 Su vida aborreció toda clase de alimento, Y se acercaron a las puertas de la muerte.
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
19 Pero a Yavé clamaron en su angustia. Él los libró de sus aflicciones.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
20 Envió su Palabra y los sanó, Y [los] libró de sus destrucciones.
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
21 ¡Den gracias a Yavé por su misericordia Y por sus maravillas para los hijos de [los ]hombres!
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
22 Ofrezcan también sacrificios de acción de gracias Y proclamen sus obras con júbilo.
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
23 Los que bajan en naves al mar, Los cuales hacen negocios sobre inmensas aguas.
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
24 Ellos vieron las obras de Yavé Y sus maravillas en las profundidades.
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
25 Porque Él habló y levantó un viento tempestuoso Que levantó las olas del mar.
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
26 Subían hacia los cielos, Bajaban a las profundidades, Su alma se derretía en su desesperación.
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
27 Temblaban y se tambaleaban como ebrios, Y toda su pericia fue inútil.
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
28 En su angustia clamaron a Yavé, Y Él los sacó de sus angustias.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
29 Calmó la tormenta De tal modo que sus olas se apaciguaron.
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
30 Entonces se alegraron porque se calmaron. Y así los guía al puerto que anhelan.
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
31 ¡Den gracias a Yavé por su misericordia, Y por sus maravillas para los hijos de [los] hombres!
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
32 Exáltenlo en la congregación del pueblo, Y alábenlo en la reunión de los ancianos.
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
33 Él cambia ríos en desierto Y manantiales de aguas en sequedales,
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
34 La tierra fructífera en estéril, Por la perversidad de los que viven en ella.
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
35 Él convierte el desierto en estanques de aguas, Y la tierra seca en manantiales.
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
36 Allí coloca a los que tienen hambre, Para que establezcan una ciudad habitada.
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
37 Siembran campos y plantan viñas Y recogen abundante fruto.
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
38 Los bendice, Y se multiplican grandemente. No permite que disminuya su ganado
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
39 Cuando son menguados y abatidos Por medio de opresión, aflicción y tristeza.
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
40 Él derrama menosprecio sobre los nobles, Y los destina a vagar errantes en un desierto.
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
41 Pero Él pone en alto a los pobres lejos de la aflicción Y hace que [sus] familias sean como un rebaño.
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
42 Los rectos lo ven y se alegran, Pero toda injusticia cierra su boca.
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
43 ¿Quién es sabio? Observe estas cosas, Y entenderá las misericordias de Yavé.
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.

< Salmos 107 >