< Salmos 107 >

1 ¡Den gracias a Yavé, Porque Él es bueno, Porque para siempre es su misericordia!
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Que lo digan los redimidos de Yavé, Los que redimió del poder del adversario,
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 Y los que congregó de las tierras, Del oriente y del occidente, del norte y del sur.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Ellos vagaron en un desierto, en región despoblada. No hallaron un camino hacia una ciudad habitada.
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Tenían hambre y sed. Sus almas desfallecían en ellos.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Pero clamaron a Yavé en su angustia. Él los libró de sus aflicciones.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 Los condujo por un camino recto Para ir a una ciudad habitada.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 ¡Den gracias a Yavé por su misericordia Y por sus maravillas para los hijos de [los ]hombres!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 Porque Él sacia al alma que tiene sed Y llena de bien al alma que tiene hambre.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Vivían en oscuridad y sombra de muerte, Prisioneros en aflicción y cadenas,
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 Por cuanto fueron rebeldes a las Palabras de ʼEL Y trataron con desprecio el consejo del ʼElyón.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Por tanto Él quebrantó sus corazones con trabajo. Cayeron y no hubo quien los ayudara.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Pero en su angustia clamaron a Yavé, Él los libró de sus aflicciones.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Los sacó de la oscuridad y de la sombra de muerte, Y rompió sus ataduras.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 ¡Den gracias a Yavé por su misericordia, Y por sus maravillas para los hijos de [los] hombres!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 Porque quebró las puertas de bronce, Y desmenuzó los cerrojos de hierro.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Fueron afligidos los necios a causa de su camino rebelde, Y a causa de sus iniquidades fueron afligidos.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 Su vida aborreció toda clase de alimento, Y se acercaron a las puertas de la muerte.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Pero a Yavé clamaron en su angustia. Él los libró de sus aflicciones.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Envió su Palabra y los sanó, Y [los] libró de sus destrucciones.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 ¡Den gracias a Yavé por su misericordia Y por sus maravillas para los hijos de [los ]hombres!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 Ofrezcan también sacrificios de acción de gracias Y proclamen sus obras con júbilo.
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Los que bajan en naves al mar, Los cuales hacen negocios sobre inmensas aguas.
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 Ellos vieron las obras de Yavé Y sus maravillas en las profundidades.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Porque Él habló y levantó un viento tempestuoso Que levantó las olas del mar.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Subían hacia los cielos, Bajaban a las profundidades, Su alma se derretía en su desesperación.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Temblaban y se tambaleaban como ebrios, Y toda su pericia fue inútil.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 En su angustia clamaron a Yavé, Y Él los sacó de sus angustias.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Calmó la tormenta De tal modo que sus olas se apaciguaron.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Entonces se alegraron porque se calmaron. Y así los guía al puerto que anhelan.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 ¡Den gracias a Yavé por su misericordia, Y por sus maravillas para los hijos de [los] hombres!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Exáltenlo en la congregación del pueblo, Y alábenlo en la reunión de los ancianos.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Él cambia ríos en desierto Y manantiales de aguas en sequedales,
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 La tierra fructífera en estéril, Por la perversidad de los que viven en ella.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Él convierte el desierto en estanques de aguas, Y la tierra seca en manantiales.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 Allí coloca a los que tienen hambre, Para que establezcan una ciudad habitada.
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 Siembran campos y plantan viñas Y recogen abundante fruto.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 Los bendice, Y se multiplican grandemente. No permite que disminuya su ganado
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Cuando son menguados y abatidos Por medio de opresión, aflicción y tristeza.
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Él derrama menosprecio sobre los nobles, Y los destina a vagar errantes en un desierto.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Pero Él pone en alto a los pobres lejos de la aflicción Y hace que [sus] familias sean como un rebaño.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Los rectos lo ven y se alegran, Pero toda injusticia cierra su boca.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 ¿Quién es sabio? Observe estas cosas, Y entenderá las misericordias de Yavé.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Salmos 107 >