< Salmos 104 >

1 Bendice, alma mía, a Yavé. ¡Oh Yavé, ʼElohim mío, cuánto te has engrandecido! Estás cubierto de esplendor y majestad.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Te cubres como con un manto de luz. Extiendes el cielo como una cortina.
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Él coloca sobre las aguas las vigas de sus altas moradas. Él convierte las nubes en su carroza. Él anda sobre las alas del viento.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Él designa los vientos como sus mensajeros, Y las llamas de fuego, como sus ministros.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Él estableció la tierra sobre sus cimientos Para que no sea sacudida.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Le colocaste como una ropa el abismo. Las aguas estaban sobre las montañas.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 A tu reprensión huyeron, Se precipitaron al estruendo de tu trueno.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Subieron las montañas, Bajaron los valles al lugar que estableciste para ellos.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Les fijaste un límite que no traspasarán, De manera que no volverán a cubrir la tierra.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Él envía manantiales por los valles. Ellos fluyen entre las montañas.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 Dan de beber a todas las bestias del campo. Mitigan su sed los asnos monteses.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Junto a ellos habitan las aves del cielo. Elevan voces entre las ramas.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Él riega las montañas desde sus altas cámaras. Con el fruto de las obras de Él está saciada la tierra.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Él desarrolla el pasto para el ganado, Y la vegetación para el servicio del hombre De tal modo que saque alimento de la tierra,
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 Y vino que alegra el corazón del hombre, El aceite para que brille su semblante Y el pan que sustenta la vida del hombre.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Los árboles de Yavé beben su savia, Los cedros del Líbano que Él plantó,
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 Donde las aves construyen sus nidos, La cigüeña, cuya casa está en los cipreses,
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Las altas montañas para las cabras monteses, Las peñas, madrigueras de los conejos.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Él hizo la luna para las estaciones. El sol conoce el punto de su ocaso.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Pones la oscuridad y es de noche. En ella corretean todos los animales del bosque.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 Los leoncillos rugen tras la presa Y buscan de ʼEL su comida.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Al salir el sol se retiran Y se echan en sus guaridas.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Sale el hombre a su trabajo, A su labor hasta el anochecer.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 ¡Cuán innumerables son tus obras, oh Yavé! Hiciste todas ellas con sabiduría. La tierra está llena de tus posesiones.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Ahí está el grande y ancho mar, Donde hay enjambre de incontables animales, Tanto pequeños como grandes.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 Allí navegan los barcos, [Y el ]cocodrilo que formaste para que juguetee en él.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Todos ellos esperan en Ti Para que les des su comida en su tiempo.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Les das, ellos recogen. Abres tu mano, Y se sacian con lo bueno.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Ocultas tu rostro Y ellos se desmayan. Les retiras su aliento, Y ellos expiran y vuelven a su polvo.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Envías tu aliento, Son creados, Y renuevas la superficie de la tierra.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 ¡Sea la gloria de Yavé para siempre! ¡Que se alegre Yavé en sus obras!
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Él mira a la tierra, Y ella tiembla, Él toca las montañas, Y ellas humean.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 A Yavé cantaré en mi vida, Mientras tenga vida cantaré salmos a mi ʼElohim.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Sea agradable a Él mi meditación. Yo me regocijaré en Yavé.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Sean exterminados de la tierra los pecadores Y los perversos dejen de ser. ¡Bendice, alma mía, a Yavé! ¡Alaben a YA!
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Salmos 104 >