< Proverbios 9 >
1 La sabiduría edificó su casa. Labró sus siete columnas.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 Degolló sus animales, Mezcló su vino, Sirvió su mesa,
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 Y envió a sus criadas A pregonarlo desde las más altas cumbres de la ciudad:
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 ¡El que sea simple, venga acá! Al falto de entendimiento le quiero hablar:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 ¡Vengan, coman de mis manjares, Y beban del vino que mezclé!
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 ¡Dejen la necedad y vivan, Pongan sus pies en el camino del entendimiento!
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 El que corrige al burlador se acarrea insultos. El que reprende al perverso se acarrea afrenta.
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 No reprendas al burlador, no sea que te aborrezca. Reprende al sabio, y te amará.
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 Da al sabio, y será aun más sabio. Enseña al justo, y aumentará su saber.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 El temor a Yavé es el principio de la sabiduría, Y el conocimiento del Santísimo es el entendimiento.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 Porque por mí se aumentarán tus días, Y años de vida se te añadirán.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 Si eres sabio, para ti mismo eres sabio, Y si eres burlador, solo tú llevarás el daño.
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 La mujer necia es alborotadora. Es simple y nada sabe.
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 Se sienta en la puerta de su casa, O en los lugares más altos de la ciudad
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 Para llamar a los que pasan, A los que van directo por sus sendas:
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 ¡Todos los ingenuos vengan acá! Y dice a los faltos de cordura:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 ¡El agua robada es dulce! ¡El pan comido en oculto es sabroso!
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 No saben ellos que allí están los muertos, Y que sus invitados están tendidos en lo profundo del Seol. (Sheol )
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )