< Proverbios 9 >

1 La sabiduría edificó su casa. Labró sus siete columnas.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 Degolló sus animales, Mezcló su vino, Sirvió su mesa,
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 Y envió a sus criadas A pregonarlo desde las más altas cumbres de la ciudad:
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 ¡El que sea simple, venga acá! Al falto de entendimiento le quiero hablar:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 ¡Vengan, coman de mis manjares, Y beban del vino que mezclé!
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 ¡Dejen la necedad y vivan, Pongan sus pies en el camino del entendimiento!
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 El que corrige al burlador se acarrea insultos. El que reprende al perverso se acarrea afrenta.
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 No reprendas al burlador, no sea que te aborrezca. Reprende al sabio, y te amará.
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 Da al sabio, y será aun más sabio. Enseña al justo, y aumentará su saber.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 El temor a Yavé es el principio de la sabiduría, Y el conocimiento del Santísimo es el entendimiento.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 Porque por mí se aumentarán tus días, Y años de vida se te añadirán.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 Si eres sabio, para ti mismo eres sabio, Y si eres burlador, solo tú llevarás el daño.
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 La mujer necia es alborotadora. Es simple y nada sabe.
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 Se sienta en la puerta de su casa, O en los lugares más altos de la ciudad
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 Para llamar a los que pasan, A los que van directo por sus sendas:
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 ¡Todos los ingenuos vengan acá! Y dice a los faltos de cordura:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 ¡El agua robada es dulce! ¡El pan comido en oculto es sabroso!
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 No saben ellos que allí están los muertos, Y que sus invitados están tendidos en lo profundo del Seol. (Sheol h7585)
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbios 9 >