< Proverbios 8 >
1 ¿No clama la sabiduría, Y el entendimiento hace oír su voz?
Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
2 En las cimas de las alturas junto al camino, En las encrucijadas de los senderos, allí está ella.
Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
3 Junto a las puertas, en la entrada de la ciudad, En el acceso a las puertas, ella da voces:
Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
4 ¡Oh hombres, a ustedes clamo! Mi voz se dirige a los hijos de los hombres.
Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
5 Oh simples, aprendan prudencia. Y ustedes, insensatos, dispongan su corazón.
Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Escuchen, porque diré cosas excelentes, Y abriré mis labios para cosas rectas.
Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Mi boca pronunciará verdad. La maldad es repugnancia para mis labios.
Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 Todas las palabras de mi boca son con justicia. En ellas nada hay torcido o perverso.
Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Son claras para el que entiende Y rectas para los que hallan el conocimiento.
Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Reciban mi enseñanza y no plata, Conocimiento, mejor que oro fino.
Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Pues mejor es la sabiduría que las perlas. Nada de lo que desees podrá compararse con ella.
Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 Yo, la sabiduría, moro con la prudencia, Y descubro el conocimiento y la discreción.
Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 El temor a Yavé es aborrecer el mal. Aborrezco la soberbia, la arrogancia, el mal camino y la boca perversa.
Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 Mío es el consejo y la eficiente sabiduría. Mía es la inteligencia y mía la valentía.
Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Por mí reinan los reyes, Y los magistrados administran justicia.
Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Por mí gobiernan los príncipes Y los nobles que juzgan la tierra.
Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Yo amo a los que me aman. Me hallan los que temprano me buscan.
Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Las riquezas y la honra están conmigo, Riquezas y justicia perdurables.
Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 Mi fruto es mejor que el oro, Aun que el oro puro, Y mi ganancia mejor que la plata escogida.
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 Yo ando por camino de justicia, Por los senderos de equidad,
Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 Para hacer que los que me aman obtengan su heredad. Y para que yo llene sus tesoros.
katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 Yavé me poseía en el principio, Ya de antiguo, antes de sus obras.
Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23 Eternamente estaba establecida, Antes de haber tierra.
Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24 Nací antes que existieran los océanos, Antes que existieran las fuentes de muchas aguas.
Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25 Antes que las montañas fueran fundadas, Antes de las colinas, fui yo engendrada.
Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26 Cuando Él no había hecho la tierra, ni los campos, Ni el primer polvo del mundo.
Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27 Cuando estableció los cielos, allí estaba yo. Cuando trazó el horizonte sobre la superficie del océano,
Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
28 Cuando afirmó los cielos arriba, Cuando afirmó las fuentes del océano,
Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
29 Cuando señaló al mar su estatuto, Para que las aguas no traspasaran su mandato, Cuando estableció los fundamentos de la tierra,
Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
30 Yo estaba junto a Él como arquitecto. Diariamente era su deleite. Me regocijaba ante Él siempre.
Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
31 Me regocijaba en su tierra habitada, Y tenía mi deleite con los hijos de los hombres.
Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32 Ahora pues, hijos, escúchenme. Inmensamente felices los que guardan mis caminos.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33 Atiendan la instrucción, sean sabios Y no la menosprecien.
Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34 ¡Inmensamente feliz es el hombre que me escucha, Que vigila en mis portones cada día, Que espera en el umbral de mis entradas!
Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35 Porque el que me halla, Halla la vida y alcanza el favor de Yavé.
Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
36 Pero el que peca contra mí, defrauda su propia alma. Todos los que me aborrecen aman la muerte.
Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.