< Proverbios 6 >
1 Hijo mío, si saliste fiador por tu prójimo, Si empeñaste tu palabra a un extraño,
Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2 Si te enredaste con tus palabras, Y quedaste atrapado con los dichos de tu boca,
basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3 Haz esto ahora, hijo mío, y líbrate. Ya que caíste en las manos de tu prójimo: Vé, humíllate e importuna a tu prójimo.
Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4 No concedas sueño a tus ojos, Ni adormecimiento a tus párpados.
Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5 Líbrate como gacela de la mano [del cazador], Como un ave de la trampa.
Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6 Mira a la hormiga, oh perezoso, Observa sus caminos y sé sabio,
Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7 La cual, sin tener jefe, Ni gobernador, ni soberano,
Hana akida, afisa au mtawala,
8 Prepara en el verano su comida. En el tiempo de la cosecha guarda su sustento.
lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9 ¿Hasta cuándo estarás acostado, oh perezoso? ¿Cuándo te levantarás de tu sueño?
Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10 Un rato duermes, otro dormitas, Un rato cruzas los brazos y descansas.
Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11 Te llega la miseria como un vagabundo, Y tu necesidad como un hombre armado.
ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12 Hombre depravado es el hombre inicuo, Que anda en la perversidad de su boca,
Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13 Guiña con un ojo, menea los pies, Hace señas con los dedos.
akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
14 En su corazón hay perversidades, Maquina maldades, y continuamente busca rencillas.
Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
15 Por tanto, su calamidad vendrá de repente. Súbitamente será quebrantado y no habrá remedio.
Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
16 Seis [cosas] aborrece Yavé, Y aun siete repugna su alma:
Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
17 Ojos altivos, boca mentirosa, Manos que derraman sangre inocente,
Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
18 Corazón que maquina planes perversos, Pies presurosos para correr al mal,
moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
19 Testigo falso que habla mentiras, Y el que enciende discordias entre sus hermanos.
shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
20 Hijo mío, guarda el mandamiento de tu padre, Y no abandones la instrucción de tu madre.
Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Átalos continuamente a tu corazón, Enlázalos en torno a tu cuello.
Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 Cuando camines, te guiarán. Cuando duermas, te protegerán. Hablarán contigo al despertar.
utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 Porque el mandamiento es lámpara, La enseñanza es luz Y camino de vida las reprensiones de la instrucción.
Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 Te guardarán de la mala mujer, De la blandura de la boca de la mujer extraña.
Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 No codicies en tu corazón su hermosura, Ni dejes que te cautive con sus párpados.
Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 Porque si la prostituta busca una hogaza de pan, La adúltera caza una vida preciosa.
Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 ¿Tomará el hombre fuego en su seno, Sin que ardan sus ropas?
Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 ¿Andará un hombre sobre brasas, Sin que se quemen sus pies?
Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 Así sucederá con el que se une a la mujer de su prójimo. Ninguno que la toque quedará impune.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 ¿No desprecian al ladrón aunque robe Para llenar su estómago cuando tiene hambre?
Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 Si es sorprendido, tiene que pagar siete veces Y entregar todo lo que tiene en su casa.
Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 Pues el adúltero es hombre sin cordura, Destructor de sí mismo es el que lo hace.
Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 Heridas y deshonra hallará, Y su afrenta no será borrada.
Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 Porque los celos son la ira del hombre. En el día de la venganza no perdonará,
Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 Ni aceptará algún rescate. No se aplacará aunque ofrezcas muchos regalos.
Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.